Kocha wa timu ya taifa ya Hispania, Luis de la Fuente, ameisifu timu yake kwa uimara na ustahimilivu baada ya kuibuka na ushindi mgumu wa bao 1-0 dhidi ya Uruguay katika mashindano ya Dunia 2026, ushindi uliowawezesha kumaliza kileleni mwa Kundi H.
Hispania ilikamilisha hatua ya makundi ikiwa na mabao matano bila kuruhusu bao hata moja, jambo lililoendeleza rekodi yao ya kutopoteza mechi kwa mfululizo wa michezo 34, huku De la Fuente akieleza kuwa hilo ni fahari kubwa kwa kikosi chake.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Hata hivyo, mchezo huo uliacha majeraha kwa baadhi ya wachezaji ambapo mshambuliaji Yeremy Pino anahofiwa kupata jeraha la mfupa na huenda akakosa mashindano yaliyosalia, huku Nico Williams akimaliza mchezo akiwa na maumivu madogo.
“Tulilazimika kupambana hadi kikomo. Wachezaji wangu walijikuta wakipitia mchezo mgumu sana kimwili, lakini walionyesha moyo wa kupambana,” alisema De la Fuente. Aliongeza kuwa hakutaka kulalamikia waamuzi bali alijikita kwenye juhudi za kikosi chake.
Kocha huyo pia alizungumzia ubora wa kiungo wake akisisitiza kuwa wachezaji kama Pedri, Fabián Ruiz, Dani Olmo, Mikel Merino na Martín Zubimendi wanaweza kubadilishana kulingana na mpinzani, huku akisema eneo la kuboresha ni kasi ya pasi na mzunguko wa mchezo.
“Nina imani kubwa na kikosi hiki. Ni timu inayotaka kuendelea kukua. Tuko kwenye njia sahihi, lakini kila mchezo unaokuja utakuwa mgumu zaidi,” alihitimisha kocha huyo.


