Kocha wa Hispania, Luis de la Fuente, amesema ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Ufaransa katika nusu fainali ya michuano ya Dunia 2026 umeonyesha kuwa kikosi chake ndicho bora zaidi duniani kwa sasa. Ushindi huo umeipeleka Hispania fainali ya michuano hiyo ikiwa imebakiza hatua moja tu kutwaa taji lake la pili la michuano ya Dunia tangu ilipotwaa ubingwa mwaka 2010.
Hispania ilidhibiti kikamilifu safu ya ushambuliaji ya Ufaransa iliyokuwa imefunga mabao 16 kabla ya mchezo huo na kutajwa kuwa moja ya safu hatari zaidi kwenye mashindano. Ufaransa haikupata hata shuti moja lililolenga lango hadi dakika za mwisho za mchezo, jambo lililoonyesha ubora wa safu ya ulinzi na mpangilio wa Hispania.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Akizungumza baada ya mechi, De la Fuente alisema kikosi chake kiliamini uwezo wake tangu mwanzo. “Niliwaambia wachezaji wangu kwamba tunacheza dhidi ya moja ya timu bora duniani, lakini wao wanacheza dhidi ya timu bora zaidi duniani. Wachezaji hawa wana vipaji, mshikamano na kujitolea, na wanafanya mambo magumu yaonekane mepesi. Tumeurudisha moyo wa Hispania ya mwaka 2010,” alisema kocha huyo.
De la Fuente alieleza kuwa mafanikio ya Hispania yanatokana na umoja na unyenyekevu wa kikosi kizima badala ya kutegemea nyota mmoja mmoja. “Jambo muhimu ni kuchagua watu sahihi wa kusafiri nao. Timu hii imejengwa na watu wenye moyo wa kusaidiana na wanaoweka maslahi ya timu mbele ya maslahi binafsi. Hata wale ambao hawakucheza walibaki kufanya mazoezi baada ya mechi, jambo linaloonyesha tabia ya kikosi hiki,” alisisitiza.
Kocha huyo pia alisema Hispania bado ina nafasi kubwa ya kuendelea kuimarika licha ya kufikisha mechi 37 mfululizo bila kupoteza na kuifikia rekodi ya Italia. “Timu hii haiachi kunishangaza. Bado tuna nafasi kubwa ya kuboresha kiwango chetu. Ningependa kucheza na Argentina fainali kutokana na urafiki wangu na Lionel Scaloni, lakini pia naiheshimu England. Nusu fainali yao inaweza kuwa kama fainali yenyewe. Fainali si kwa ajili ya kushinda tu, bali pia kufurahia safari tuliyopitia, na taji litakuwa zawadi ya kazi yetu,” alihitimisha.


