Kiungo wa Argentina, Rodrigo De Paul, amesema nahodha wao Lionel Messi anafurahia kwa kiwango kikubwa kwenye michuano ya Dunia 2026, jambo linalowapa nguvu wachezaji wenzake kabla ya mchezo wa nusu fainali dhidi ya England. Argentina, ambayo ni mabingwa watetezi, itakutana na England Jumatano katika mchezo unaotarajiwa kuwa wa ushindani mkubwa.
Messi ameandika historia mpya kwenye michuano hii baada ya kuvunja rekodi mbalimbali, ikiwemo kuwa mchezaji mwenye idadi kubwa zaidi ya mechi za michuano ya Dunia na kuongeza rekodi yake ya mabao hadi kufikisha 21 katika fainali hizo. Katika michuano ya Dunia 2026 linalofanyika Canada, Mexico na Marekani, nyota huyo wa Inter Miami amefunga mabao nane na kuendelea kuonyesha kiwango cha juu akiwa na umri mkubwa.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Akizungumzia hali ya Messi, De Paul alisema kuona nahodha huyo akiwa na furaha ni jambo linalompa faraja kutokana na safari ndefu aliyopitia akiwa na jezi ya Argentina. “Kumuona akifurahia mchezo kunanifanya nijisikie vizuri sana, ukizingatia kila kitu alichopitia na kila kitu alichopigania akiwa na jezi hii. Nafikiri michuano hii ya Dunia limemfanya afurahie soka kwa dhati,” alisema De Paul.

Akizungumzia mchezo dhidi ya England, De Paul alikiri kuwa Argentina inaiheshimu timu hiyo kutokana na ubora wa wachezaji wake pamoja na kocha wao. “Tuna wasiwasi kwa sababu tunakutana na timu kubwa yenye wachezaji wengi bora na kocha mzuri. Lakini wasiwasi huo unatufanya tuwe makini zaidi na kuhakikisha tunajiandaa vizuri,” alisema.
De Paul amesema kuwa kufika hatua moja kabla ya fainali ni motisha kubwa, lakini anaamini mechi kama hizi huamuliwa na mambo madogo.“Kila mchezo wa michuano ya Dunia ni kama fainali. Tunajua haitakuwa rahisi, lakini tunataka kufurahia wakati huu na kubaki watulivu. Mwisho wa siku, mashindano makubwa kama haya huamuliwa na maelezo madogo,” alihitimisha.


