Kiungo wa kimataifa wa Uingereza nayekipga kwenye klabu ya Everton Dele Alli a,efanikiwa kupata namba uake ya bahati ambayo alikuwa akivaa kwenye klabu ya Tottenham Hotspurs jersey namba 20.
Wakati Dele Alli anasajiriwa na klabu ya Everton hakuweza kuipata jersey namba hiyo ambayo ilikuwa inavaliwa na Cenk Tosun ambaye kwa sasa ameondoka kwenye klabu hiyo na badala yake alipewa jeresy namba 36.
Dele Alli anatumaini kuwa kubalisha kwa jersey namba kutoka 36 hadi 20 kutamfanya aweze kurudisha makali yake aliyokuwa nayo kwenye kikosi cha Spurs na atapata muda wa kucheza mara kwa mara kwenye kikosi hicho.
Dele Alli alisajiriwa na klabu ya Everton akitokea klanu ya Tottenham Hotspur kwenye usajiri wa dirisha dogo la usajiri wa mwezi january baada ya kokesa nafasi ya kucheza mara kwa kwa mara kwenye kikosi cha Spurs.