Bodi ya Ligi Kuu Tanzania TPLB imetangaza washindi wa tuzo za mwezi Februari kwa msimu wa 2025/26.Mshambuliaji wa Yanga SC, Laurindo Dilson Depu, amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa Mwezi Februari baada ya kuonyesha kiwango bora cha uchezaji.
Depu alifunga mabao mawili katika michezo miwili aliyoshiriki na kusaidia Yanga kusalia kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya NBC. Katika fainali ya tuzo hizo, aliwashinda beki wa Simba SC, Rushine De Reuck, na kiungo Azam FC, Idd Selemani ‘Nado’.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kwa upande wa makocha, Steve Barker wa Simba SC amechaguliwa kuwa Kocha Bora wa Mwezi Februari. Barker aliiongoza timu yake kushinda michezo miwili na kutoa sare moja, hatua iliyosaidia Simba kupanda kutoka nafasi ya sita hadi ya tatu kwenye msimamo wa ligi. Aliingia fainali ya tuzo hiyo akishindana na Pedro Goncalves wa Yanga SC na Florent Ibenge wa Azam FC.
Tuzo hizi zinatolewa na Kamati ya Tuzo za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kama kutambua wafanyakazi wa ligi walioonyesha ubora katika kila mwezi wa mashindano.

