Kiungo wa England, Eberechi Eze amewataka wachezaji wenzake kupuuza wakosoaji wa nje baada ya sare ya bila mabao dhidi ya Ghana kwenye michuano ya Dunia, akisisitiza kuwa timu inapaswa kubaki imara na yenye utulivu licha ya matokeo hayo.
Akizungumza na waandishi wa habari, Eze alisema “Ni kawaida, kutakuwa na maoni kutoka nje kuhusu kile kinachotokea na kile wanachofikiri kuhusu mchezo, lakini hatujazingatia sana hilo. Tunaamini kile tunachofanya.” Aliongeza kuwa timu haiwezi kutumia muda mwingi kusikiliza watu ambao hawapo uwanjani.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Eze alisisitiza umuhimu wa kujiamini na kudumisha mtazamo chanya ndani ya kikosi cha England national football team, akisema: “Hatuwezi kutumia muda mwingi kusikiliza watu ambao hawachezi wala hawapo uwanjani. Tunajua tunachokifanya na tuna imani nacho, hivyo hilo ndilo jambo muhimu.”
Timu ya England ilitawala mchezo kwa kumiliki mpira kwa asilimia 78.8 katika mechi hiyo iliyochezwa Boston Stadium, lakini haikuweza kupata bao licha ya mashambulizi mengi na mpira kugonga mwamba wa goli. Nahodha Harry Kane pia alikosa nafasi muhimu dakika za mwisho.
Licha ya matokeo hayo, Eze alibaki na mtazamo chanya akisema: “Ni safari ndefu, huwezi kuwa juu sana au chini sana. Tunapaswa kuamini tunachokifanya na kuendelea kuwa na matumaini kuelekea mchezo ujao dhidi ya Panama,” akisisitiza kuwa England bado ina nafasi nzuri ya kumaliza kinara wa kundi.


