Uongozi wa Feyenoord unatajwa kuwa katika hatua za mwisho za kufanya mazungumzo ya kumrudisha aliyekuwa kocha wao, Arne Slot, kufuatia kuondolewa kwa Robin van Persie kwenye nafasi ya kocha mkuu wa klabu hiyo ya Uholanzi.
Van Persie, ambaye ni mmoja wa magwiji wakubwa katika historia ya soka la Uholanzi, amefutwa kazi baada ya viongozi wa klabu kufanya tathmini ya kina kuhusu mwenendo wa timu hiyo, licha ya kufanikiwa kuifikisha Feyenoord katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
“Viongozi hawakuridhishwa na kiwango cha uchezaji pamoja na idadi ya pointi ambazo timu ilikuwa ikikusanya katika mechi mbalimbali,” chanzo cha karibu na klabu hiyo kilieleza, kikibainisha kuwa maamuzi hayo yalifikiwa baada ya mfululizo wa matokeo yasiyoridhisha.
Kwa sasa, Arne Slot yupo huru baada ya kuachana na Liverpool, jambo ambalo limeifanya Feyenoord kuona fursa nzuri ya kumrejesha kocha huyo aliyewahi kuipa mafanikio makubwa klabu hiyo kabla ya kuhamia England. “Slot anaeleweka vizuri ndani ya klabu na anabaki kuwa chaguo linalopendwa na mashabiki wengi,” kiliongeza chanzo hicho.



