Giroud Akiwasha Dhidi ya Sevilla,Champions League.

Olivier Giroud alikuwa shujaa wa mechi ya Chelsea kwa mara ya pili katika michezo mingi ya Ligi ya Mabingwa kwani alifunga mabao yote manne katika ushindi wa 4-0 dhidi ya Sevilla na kushika nafasi ya kwanza katika Kundi E.

Giroud Akiwasha Dhidi ya Sevilla,Champions League.

Giroud, ambaye alicheza kwa kuanza katika mechi yake ya 50 kwa Chelsea, alikuwa katika kiwango bora wakati akifanikiwa kufunga mabao 10 katika mechi saba za ugenini kwenye mashindano na kuhakikisha Chelsea inakwenda raundi ya 16.

Sevilla walienda kwenye mchezo huu wakiwa na rekodi ya kutofungwa katika mechi 14 za nyumbani kwenye mashindano yote ya Ulaya lakini rekodi yao ilivunjwa na timu ya Frank Lampard inayofanya kazi kwa bidii, ambayo ilicheza kwa kuzuia lakini ilishambulia kwa ufasaha.

Baada ya kufunga kwa miguu yote, Giroud alifunga kwa kichwa cha juu na kisha akafunga kwa mkwaju wa penati pia amekuwa mchezaji mkongwe zaidi kufunga hat-trick ya Ligi ya Mabingwa, akiwa na miaka 34 na siku 63.

Kai Havertz aliruhusiwa kuipita safu ya ulinzi ya Sevilla na kupiga mpira kwa Giroud, ambaye aligusa kuudhibiti kabla ya kufungua mwili wake na kupiga kwenye kona ya mbali ya wavu kutoka yadi 12.

Franco Vazquez akaokoa mpira wa kichwa cha nguvu kutoka kwa Antonio Rudiger nje ya mstari, ndani ya kipindi cha kwanza wakati Sevilla ikijaribu kumiliki mpira.

Lakini Giroud alifunga tena katika dakika 54, baada ya kupata pasi ya Mateo Kovacic kabla ya kumpita Sergi Gomez na kupiga shuti juu ya Pastor.

N’Golo Kante, kama mbadala, alicheza upande kulia na zikiwa zimesalia dakika 16 mpira kumalizika alipiga krosi safi iliyounganishwa na kichwa cha Giroud na kufanya Giroud afunge hat-trick.

Mshindi wa Kombe la Dunia akiwa na Ufaransa alifunga goli la nne kwa penati dakika za mwishoni na kukamilisha usiku wa kihistoria.


FURAHIA MUZIKI MTANDAONI HUKU UKITENGEZA MKWANJA!!

Mchezo wa Astro Legend unakupatia burudani ya muziki kupitia kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Utaburudika huku ukiendelea kutengeza mkwanja mrefu, jiunge sasa na uwe miongoni mwa mabingwa!!

INGIA MCHEZONI

32 Komentara

    Kwa kweli Chelsea walijua kunifurahisha haswa mchezaji Giroud alikuwa hatari kwenye lango alionyesha uwezo wake ingawa walikuwa wanasema ni mzee ila alijua kuishambulia Seville vilivyo

    Jibu

    Duh!!!mbona mambo

    Jibu

    Safi

    Jibu

    Giroud noma sana

    Jibu

    Vizuri walijua kupambana sana

    Jibu

    Giroud ni mchezaji mzuri Sana

    Jibu

    Chelsea jana wameonyesha wapo vizuri

    Jibu

    Chelsea wapo vizuri

    Jibu

    Giroud bado anadhihirisha kuwa Tammy Abraham bado anavingi vya kujifunza kutoka kwake nadhani ni somo zuri sana kwa Tammy.

    Jibu

    Giround bado ana kibarua kizito sana

    Jibu

    Inapendeza san

    Jibu

    Yuko vizuri sana kijana.

    Jibu

    Chelsea walijitahidi sana kucheza vizuri

    Jibu

    Bull striker

    Jibu

    Kijana yupo vzr

    Jibu

    Chelsea wapo vizur

    Jibu

    Safi sana

    Jibu

    Credit kwake giroud halikuwah kwny ubora wa Hali ya juu kwny mchezo wa jana zidi ya sevilla

    Jibu

    Baada ya kufunga kwa miguu yote, Giroud alifunga kwa kichwa cha juu na kisha akafunga kwa mkwaju wa penati pia amekuwa mchezaji mkongwe zaidi kufunga hat-trick ya Ligi ya Mabingwa, akiwa na miaka 34 na siku 63.

    Jibu

    Mechi hii Chelsea walinifurahish Sana kwa kidedea Hilo nice Chelsea.

    Jibu

    Daah !! Mambo hayo.

    Jibu

    Huyu ndio giroud tunaemfaham

    Jibu

    Safi

    Jibu

    Yupo vzr kijana

    Jibu

    Alfanya poa sana

    Jibu

    Safi

    Jibu

    Safi sana

    Jibu

    Huyo ndo Giroud sasa ,hakipata nafasi halembi

    Jibu

    Safi sanaaa

    Jibu

Acha ujumbe