Beki wa Liverpool fc, Joe Gomez amesema kipigo cha mabao 4-2 walichopata dhidi ya Aston Villa kimewaumiza sana huku akiwataka wachezaji wenzake kuhakikisha wanamaliza msimu kwa ushindi dhidi ya Brentford fc. ili kujihakikishia nafasi ya kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Matokeo hayo yameishusha Liverpool hadi nafasi ya tano kwenye msimamo wa Ligi Kuu England, huku wakikabiliwa na presha kutoka kwa AFC Bournemouth na Brighton & Hove Albion katika mbio za kumaliza ndani ya nafasi tano bora.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Villa waliutumia vibaya udhaifu wa safu ya ulinzi ya Liverpool kwa kufunga mabao manne, huku timu hiyo ya Merseyside ikipata pointi moja pekee katika michezo yake mitatu ya mwisho ya ligi.
“Inasikitisha kwa sababu ni makosa ya umakini mdogo. Premier League ina tofauti ndogo sana na hilo linaongeza maumivu,” alisema Gomez kupitia tovuti rasmi ya klabu hiyo.
“Hatuwezi kukaa na kujionea huruma. Tunajua tunachotakiwa kufanya wiki ijayo na tunapaswa kuifunga Brentford nyumbani,” aliongeza.
Gomez pia amesema Liverpool wanahitaji kuwapa mashabiki sababu ya kujivunia kwa namna wanavyocheza, huku timu hiyo inayofundishwa na Arne Slot ikitarajiwa kumaliza msimu bila taji lolote.


