Mason Greenwood anaendelea kuwa gumzo kubwa katika soka la Ulaya baada ya msimu wake bora akiwa Marseille. Nyota huyo wa England ameonyesha kiwango cha juu nchini Ufaransa kiasi kwamba kocha wa Atletico Madrid, Diego Simeone, amemtaja kuwa mshambuliaji anayefaa kabisa katika mfumo wake wa mchezo. Hali hiyo imeanzisha vita vipya vya usajili kabla ya dirisha kubwa la majira ya kiangazi kufunguliwa.

Simeone amekuwa akimfuatilia Greenwood tangu alipocheza kwa mkopo Getafe kwenye La Liga, ambako alionyesha uwezo mkubwa wa kucheza katika mazingira ya soka la Hispania. Uwezo wake wa kucheza maeneo tofauti ya ushambuliaji, kasi yake pamoja na umaliziaji wake wa hatari vimeifanya Atletico kuona kuwa anaweza kuwa muhimu kwa safu ya ushambuliaji.
Hata hivyo, Marseille hawana haraka ya kumuachia nyota wao huyo. Baada ya kufunga mabao 26 na kutoa asisti 11 katika mechi 45 za mashindano mbalimbali msimu huu, klabu hiyo imeweka thamani inayoweza kufikia euro milioni 100 kwa mchezaji huyo. Kiwango hicho kimemfanya kuwa mmoja wa washambuliaji wanaotafutwa zaidi barani Ulaya kwa sasa.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Mustakabali wa Greenwood unaweza pia kuathiriwa na hatma ya Julian Alvarez ndani ya Atletico Madrid. Kumekuwa na tetesi za muda mrefu zinazomhusisha Alvarez na Barcelona, na iwapo ofa kubwa itawasilishwa, Atletico inaweza kupata fedha za kutosha kufanikisha usajili wa Greenwood.

Wakati Atletico Madrid wakipanga mkakati wao, Roma nao wameingia kwenye mbio za kumuwania mshambuliaji huyo. Aidha, Manchester United wanaendelea kufuatilia kwa karibu maendeleo hayo kutokana na kipengele cha kupata asilimia 40 ya fedha za mauzo ya baadaye walichoweka walipomuuza Marseille mwaka 2024. Hivyo, ikiwa vita ya usajili itapandisha bei ya Greenwood hadi kiwango hicho kikubwa, United nao wanaweza kunufaika kwa kiasi kikubwa.



