Mshambuliaji wa Sweden, Viktor Gyokeres, amesema timu yake italazimika kucheza kwa kiwango cha juu sana, hasa katika safu ya ulinzi, ikiwa inataka kufanya maajabu kwa kuiondoa Ufaransa katika hatua ya 32 bora ya mashindano ya Dunia. Sweden itavaana na makamu bingwa wa michuano ya Dunia 2022 siku ya Jumanne mjini New Jersey katika mechi inayotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.
Akizungumza katika kambi ya mazoezi ya Sweden iliyopo Dallas, nyota huyo wa Arsenal alisema kazi iliyo mbele yao si rahisi. “Tutalazimika kuwa katika kiwango chetu bora. Ni lazima mpangilio wetu wa kujilinda uwe karibu na ukamilifu, kisha tutumie vizuri nafasi chache tutakazozipata,” alisema Gyokeres.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Sweden ilifanikiwa kufuzu hatua ya mtoano baada ya kuifunga Tunisia mabao 5-1, kupokea kipigo cha mabao 5-1 kutoka Uholanzi na kutoka sare ya 1-1 dhidi ya Japan. Licha ya matokeo hayo yaliyobadilika-badilika, Gyokeres amesema kikosi hicho bado kina imani kubwa ya kufanya vizuri dhidi ya moja ya timu bora duniani.

Gyokeres pia alisema anatarajia kwa hamu kukutana na beki mwenzake wa Arsenal, William Saliba, ambaye atakuwa akiichezea Ufaransa. Wakati huo huo, Ufaransa inaingia katika mchezo huo ikiwa na morali kubwa baada ya kushinda mechi zote tatu za hatua ya makundi, huku Kylian Mbappe na Ousmane Dembele wakifunga mabao manne kila mmoja na kuifanya timu hiyo kuwa miongoni mwa vinara wa kutwaa taji la Dunia.


