Hossam Hassan Aishutumu VAR na Waamuzi Baada ya Misri Kutolewa na Argentina

Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Misri, Hossam Hassan, amesema hatatazama tena mechi zozote za michuano ya Dunia 2026 baada ya timu yake kuondolewa kwa maumivu na mabingwa watetezi Argentina katika hatua ya 16 bora. Misri ilikuwa mbele kwa mabao 2-0 hadi dakika ya 79 kabla ya Argentina kufanya comeback ya kushangaza na kushinda kwa mabao 3-2.

Hossam Hassan Aishutumu VAR na Waamuzi Baada ya Misri Kutolewa na Argentina
Akizungumza kwa hasira baada ya mchezo huo, Hassan aliwashutumu waamuzi kwa kile alichokiita maamuzi yasiyo ya haki yaliyoinyima Misri ushindi. “Ninarudi nyumbani na sitatazama tena mechi yoyote ya mashindano haya. Kilichotokea kwetu si haki. Tulistahili kupewa penalti, tulifunga bao ambalo lilikataliwa, na sijui kwa nini lilikataliwa,” alisema Hassan.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Bao la Mostafa Zico lililofungwa dakika ya 62 lilibatilishwa baada ya ukaguzi wa VAR kubaini kuwa kulikuwa na madhambi katika maandalizi ya bao hilo. Aidha, Misri ilidai ilinyimwa penalti kufuatia Hamdy Fathy kuvutwa ndani ya eneo la hatari, kabla ya Argentina kufunga bao la ushindi dakika ya 92 na kuzima ndoto za Wamisri kufuzu robo fainali.

Hossam Hassan Aishutumu VAR na Waamuzi Baada ya Misri Kutolewa na ArgentinaHassan alisisitiza kuwa, licha ya makosa yaliyofanywa na wachezaji wake, kilichoumiza zaidi ni maamuzi ya waamuzi. “Ninachukia kupoteza, lakini kinachoniumiza zaidi ni kupoteza kwa namna isiyo ya haki. Mashabiki wasihuzunike, tulifanya kila tuwezalo kuwapa furaha. Kilichonifurahisha ni kwamba wachezaji wangu walifuata mpango wa mchezo na walipambana kwa kiwango cha juu,” alisema.

Hossam Hassan Aishutumu VAR na Waamuzi Baada ya Misri Kutolewa na ArgentinaKocha huyo aliwapongeza wachezaji wake kwa ushindani waliouonyesha dhidi ya Argentina, akibainisha kuwa wengi wao wanacheza ligi ya ndani ya Misri tofauti na mataifa mengi yenye wachezaji wanaocheza Ulaya. “Nimeridhishwa sana na juhudi zao. Isipokuwa Mohamed Salah na Omar Marmoush, wengi wa wachezaji wetu wanatoka ligi ya ndani, lakini bado tuliweza kushindana na timu yoyote duniani,” alihitimisha Hassan.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.