Infantino Asalimu Amri, Afuta Mpango wa Kuuza Hisa za Michuano ya Dunia

Rais wa FIFA, Gianni Infantino, ameondoa rasmi pendekezo lake la kuuza hisa za taji la Dunia kupitia kampuni ya uwekezaji ya thamani ya dola bilioni 20, baada ya kukumbana na upinzani mkubwa kutoka ndani ya FIFA na vitisho vya mataifa ya Ulaya kususia mpango huo.

Infantino Asalimu Amri, Afuta Mpango wa Kuuza Hisa za Michuano ya DuniaInfantino alikuwa amependekeza kuanzishwa kwa kampuni itakayoshirikisha wawekezaji binafsi, akiwemo familia ya Kushner, ili kuendesha shughuli za taji la Dunia. Hata hivyo, mpango huo ulipingwa vikali tangu ulipotangazwa, huku nchi zote 55 wanachama wa UEFA zikidaiwa kuwa tayari kususia mashindano ya FIFA endapo ungeendelea.

mpira wa miguu, kubeti mpira wa miguu, bashiri soka, soka, beti kwenye soka, odds za soka, bashiri mpira wa miguu, beti za soka, beti mechi za soka, odds za kubeti mpira wa miguu

Shinikizo liliongezeka zaidi baada ya maafisa wawili waandamizi wa FIFA kuukosoa hadharani mpango huo. Mmoja wao, Carlos Cordeiro, alijiuzulu nafasi yake ya mshauri wa Rais wa FIFA akieleza kuwa hawezi kuunga mkono hatua ya kuuza sehemu ya umiliki wa taji la Dunia, huku Afisa Mkuu wa Uendeshaji wa FIFA, Kevin Lamour, akidai wafanyakazi walidanganywa kutokana na ukosefu wa uwazi katika maandalizi ya mpango huo.

Infantino Asalimu Amri, Afuta Mpango wa Kuuza Hisa za Michuano ya DuniaKatika taarifa yake ya Ijumaa jioni, Infantino alisema baada ya kusikiliza maoni ya wadau mbalimbali imeonekana wazi kuwa pendekezo hilo limeleta mgawanyiko mkubwa kuliko manufaa yaliyotarajiwa, hivyo halitaendelea.

Infantino Asalimu Amri, Afuta Mpango wa Kuuza Hisa za Michuano ya Dunia“Baada ya kusikiliza kwa makini maoni yote, imebainika wazi kuwa mradi huo umeleta migawanyiko ambayo haitasaidia tena kufikia lengo lililokusudiwa hapo awali. Kwa hiyo, pendekezo hilo halitaendelezwa,” amesema Gianni Infantino. Naye Carlos Cordeiro aliongeza, “Siwezi kukaa kimya huku FIFA ikifikiria kuuza hisa katika taji  la Dunia,” huku Kevin Lamour akisisitiza kuwa, “Huu ni mradi wa mtu mmoja… sasa ni wakati wa viongozi kufanya maamuzi sahihi.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.