Klabu ya Aston Villa imekamilisha usajili wa kiungo wa kimataifa wa Brazil, João Gomes, kutoka Wolverhampton Wanderers (Wolves) kwa ada inayokadiriwa kufikia pauni milioni 35. Kiungo huyo amejiunga na Villa Park baada ya kusaini mkataba wa miaka mitano, akianza rasmi safari mpya chini ya kocha wa Aston Villa.
Usajili wa Gomes unakuja baada ya Wolves kushuka daraja mwishoni mwa msimu uliopita, hali iliyofungua mlango kwa Villa kumsajili mmoja wa viungo waliokuwa wakitegemewa zaidi ndani ya kikosi hicho. Aston Villa inaamini kuwa mchezaji huyo ataleta nguvu mpya katikati ya uwanja kutokana na uwezo wake wa kukaba, kupokonya mipira na kuanzisha mashambulizi.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
“Ninafurahia kujiunga na Aston Villa. Ni hatua kubwa katika maisha yangu ya soka na nipo tayari kutoa kila kitu kwa ajili ya klabu na mashabiki,” Gomes alinukuliwa akisema baada ya kukamilisha usajili wake.
Kwa upande wake, Aston Villa ilieleza kuwa usajili wa João Gomes ni sehemu ya mpango wa kuimarisha kikosi kuelekea msimu mpya. “João ni kiungo mwenye ubora, nguvu na uzoefu wa kucheza katika kiwango cha juu. Tunaamini atakuwa sehemu muhimu ya mafanikio yetu,” ilieleza taarifa ya klabu.
João Gomes anatarajiwa kuziba pengo lililoachwa na Youri Tielemans aliyehamia Manchester United pamoja na Amadou Onana ambaye kwa sasa yupo nje ya uwanja kutokana na jeraha la goti. Mashabiki wa Aston Villa sasa watakuwa na matumaini makubwa kwamba kiungo huyo wa Brazil ataongeza ushindani na uimara katika safu ya kati ya timu hiyo.


