Juventus Yabeba Copa Italia Kwa Mara Ya 14

Timu ya Juventus imefanikiwa kubeba kombe la Coppa Italia kwa mara ya 14 sasa baada ya ushinda wa 2-1 dhidi ya Atalanta hapo jana.

Katika mechi iliyoonekana kuwa na usawa huku timu zote zikishambulia kwa wakati tofauti tofauti, Mabingwa wa Kihistoria wa Serie A walikuwa washindi kwa magoli ya Kulusevski na Chiesa, huku Morata akionekana kupoteza magoli ya wazi mara kadhaa katika mchezo huo.

Ushindi huo wa jana umewafanya Vijana wa Turin kuchukua kombe hilo kwa mara ya 14 sasa na kuweka rekodi ya kuwa timu iliyochukua kombe hilo kwa mara nyingi zaidi, ikifuatiwa na As Roma waliobeba mara tisa.

Katika mchezo huo wachezaji wa Juventus, Cuadrado, Chiesa na Kulusevski waling’aa kwa kuonesha mchezo mzuri sana kwa nafasi zao. Kombe hilo lilifurahiwa sana na wachezaji wa Juventus kutokana na ukweli kuwa msimu huu umekuwa msimu mgumu kwa wana hawa wa Turin.

UNAWEZA KUWA MILIONEA WAKATI WOWOTE!

Zungusha na ushinde mkwanja wako papo hapo baada ya mzunguko kukamilika. Ni kugusa tu 🤑.

BASHIRI SASA

2 Komentara

    Pongezi kwao

    Jibu

    Safi sana

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.