Lewandowski Avunja Rekodi ya Messi Barcelona, Baada ya Kuzifunga Timu 41 Tofauti

Mshambuliaji wa FC Barcelona, Robert Lewandowski, ameandika historia mpya katika michuano ya UEFA Champions League baada ya kufunga dhidi ya timu 41 tofauti.

Kwa mafanikio hayo, Lewandowski amemzidi nyota wa zamani wa FC Barcelona, Lionel Messi, ambaye aliwahi kushikilia rekodi hiyo kwa kufunga dhidi ya timu 40 tofauti katika mashindano hayo.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa  

Rekodi hiyo inamweka Lewandowski kuwa mchezaji pekee aliyewahi kufunga dhidi ya idadi kubwa zaidi ya timu katika historia ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, jambo linalothibitisha uimara na ubora wake wa muda mrefu katika soka la kiwango cha juu.

Lewandowski Avunja Rekodi ya Messi Barcelona, Baada ya Kuzifunga Timu 41 TofautiKatika mafanikio hayo, mshambuliaji huyo raia wa Poland amefunga mabao dhidi ya timu kutoka mataifa mbalimbali ikiwemo England, Hispania, Italia, Ujerumani, Ufaransa, Ureno na Uholanzi, pamoja na nchi nyingine nyingi za Ulaya.

Uwezo huo unaonyesha uimara wake katika mazingira tofauti ya ushindani, huku Lewandowski akiendelea kujiweka miongoni mwa washambuliaji bora zaidi kuwahi kutokea katika historia ya soka duniani.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.