Klabu ya Liverpool inadaiwa kuanza mazungumzo ya siri na kocha mkuu wa Bournemouth, Andoni Iraola, huku mustakabali wa kocha wao Arne Slot ndani ya Anfield ukiendelea kuwa shakani kuelekea mwisho wa msimu wa Ligi Kuu England.
Shinikizo limeongezeka kwa Slot mwenye umri wa miaka 47 baada ya Liverpool kupokea kipigo cha mabao 4-2 dhidi ya Aston Villa, matokeo yaliyoiweka timu hiyo katika hatari ya kukosa nafasi ya kushiriki UEFA Champions League msimu ujao.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Hali imeendelea kuwa mbaya zaidi baada ya mshambuliaji nyota wa Liverpool, Mohamed Salah, kuchapisha ujumbe wenye utata kupitia mitandao ya kijamii, hatua iliyotafsiriwa na wengi kuwa ishara ya kutokuwa na uhakika kuhusu mustakabali wake ndani ya klabu hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka FootMercato, viongozi wa Liverpool wanatajwa kupanga kumfuta kazi Slot baada ya kushindwa kutetea ubingwa wa Ligi Kuu England licha ya klabu kutumia fedha nyingi kusajili wachezaji wapya msimu uliopita.
“Liverpool wanafikiria kufanya mabadiliko ya benchi la ufundi ikiwa timu itashindwa kufuzu Ligi ya Mabingwa Ulaya, huku Andoni Iraola akiwa mmoja wa makocha wanaopewa nafasi kubwa kuchukua jukumu hilo,” zimeeleza taarifa hizo.


