Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, amefanya ukaguzi wa maendeleo ya ukarabati unaoendelea katika viwanja vya michezo vya Benjamin Mkapa na Uhuru jijini Dar es Salaam.
Katika ukaguzi huo uliofanyika Machi 13, 2026, Makonda alitembelea Uwanja wa Benjamin Mkapa na kujionea maendeleo ya kazi mbalimbali zinazofanyika, ikiwemo zoezi la ufungaji wa viti vipya katika majukwaa ya uwanja huo.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Makonda amemtaka mkandarasi anayesimamia mradi huo kuongeza kasi ya kazi ili kukamilisha ufungaji wa viti kwa wakati uliopangwa.
Amesema kukamilika kwa maboresho hayo kutasaidia uwanja huo kuwa na hadhi ya kimataifa na kuweza kutumika katika mashindano makubwa ya michezo pamoja na matukio mengine muhimu ya kitaifa.
Aidha, Makonda amesisitiza kuwa Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya michezo nchini ili kuhakikisha Tanzania inakuwa na viwanja vinavyokidhi viwango vya kimataifa.

