Klabu ya Manchester City imethibitisha kuwa jukwaa jipya la Kaskazini ndani ya Uwanja wa Etihad Stadium sasa litajulikana kama “The Pep Guardiola Stand” kwa heshima ya kocha wao mkuu, Pep Guardiola.
Uamuzi huo umeelezwa kuwa ni ishara ya kutambua mchango mkubwa wa Guardiola ambaye ameiongoza City kwa kipindi cha miaka 10 yenye mafanikio makubwa katika historia ya klabu hiyo ya England.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Jukwaa hilo lililofanyiwa upanuzi linatarajiwa kufunguliwa rasmi kwa uwezo wake wote Jumapili hii, wakati Manchester City itakapowakaribisha Aston Villa katika mchezo wa mwisho wa Guardiola akiwa kocha wa timu hiyo.
Katika kipindi chake ndani ya City, Guardiola ameisaidia timu hiyo kutwaa mataji mbalimbali ya ndani na kimataifa, huku akitajwa kuwa mmoja wa makocha walioibadilisha zaidi klabu hiyo kisoka na kiushindani.
“Kuitwa kwa jukwaa hili kwa jina la Pep Guardiola ni sehemu ya kuthamini mchango wake mkubwa na mafanikio aliyoiwekea Manchester City kwa miaka yote aliyohudumu klabuni,” ilieleza taarifa ya klabu hiyo.


