Manchester United imeweka rasmi jina la winga wa AC Milan na timu ya taifa ya Ureno, Rafael Leão, katika orodha yake ya wachezaji wanaowahitaji kuelekea msimu ujao wa usajili.
Kwa mujibu wa ripoti mbalimbali za vyombo vya habari, Leão anaweza kupatikana kwa ada ya chini zaidi kufuatia AC Milan kushindwa kufuzu Ligi ya Mabingwa Ulaya, jambo ambalo limefungua milango kwa klabu kadhaa kubwa Ulaya kuanza mazungumzo.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Hata hivyo, changamoto kubwa katika dili hilo inatajwa kuwa mshahara wake, ambapo anataka zaidi ya pauni 200,000 kwa wiki, hali inayoweza kuleta mvutano katika mazungumzo ya usajili.

Leão, ambaye kwa sasa yupo Marekani akiwa na timu ya taifa ya Ureno, ameripotiwa kunukuliwa akisema “Ninatafuta changamoto mpya katika klabu yenye malengo ya kushinda mataji makubwa ya Ulaya,” kauli ambayo imezidi kuchochea vita ya usajili kati ya vigogo wa soka la Ulaya. Mkataba wake na AC Milan unaendelea hadi Juni 30, 2028, lakini mustakabali wake unatarajiwa kuwa gumzo kubwa katika dirisha lijalo la usajili.


