Mangungu Aibuka Kivingine

Mwenyekiti wa Simba SC, Murtaza Mangungu, amesema uongozi wa klabu hiyo utaendelea kuimarisha kikosi kuelekea msimu wa 2026/27, huku ukishirikiana kwa karibu na benchi la ufundi kuhakikisha timu inakuwa imara zaidi kwa mashindano ya ndani na kimataifa.

Mangungu Aibuka Kivingine

Mangungu amesema tayari benchi la ufundi limewasilisha mapendekezo kuhusu maeneo yanayohitaji kuongezewa nguvu, na uongozi umeanza kuyafanyia kazi ili kuhakikisha Simba inaingia msimu mpya ikiwa na kikosi chenye ushindani mkubwa.

Ameeleza kuwa mafanikio ya msimu uliopita, yaliyoshuhudia Simba ikitwaa mataji ya Kombe la Muungano na Kombe la Shirikisho la CRDB, yameongeza ari ya kufanya maboresho zaidi badala ya kuridhika na mafanikio hayo.

Mangungu Aibuka Kivingine

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

“Simba ya sasa ni timu nzuri, lakini lengo letu ni kuifanya iwe bora zaidi. Tunataka kuhakikisha tunakuwa na kikosi chenye uwezo mkubwa wa kushindana na kufikia malengo makubwa zaidi msimu ujao,” amesema Mangungu.

Mangungu Aibuka Kivingine

Amesema ushirikiano mzuri uliopo kati ya uongozi na benchi la ufundi umeifanya mipango ya usajili na maandalizi ya msimu mpya kwenda kwa utaratibu unaotakiwa, huku kila hatua ikichukuliwa kwa kuzingatia maslahi ya klabu na malengo ya kuijenga Simba yenye ushindani wa hali ya juu.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.