Nahodha wa Argentina, Lionel Messi, amesema ana matarajio makubwa ya kuivaa England katika mchezo wa nusu fainali ya michuano ya Dunia 2026, akieleza kuwa itakuwa mara yake ya kwanza kucheza dhidi ya taifa hilo katika mashindano makubwa na kwamba ni moja ya mechi maalumu zaidi katika maisha yake ya soka.
Argentina ilitinga hatua hiyo baada ya kuichapa Uswisi mabao 3-1 kufuatia muda wa nyongeza, ushindi uliowapa tiketi ya kuendelea na safari ya kutetea ubingwa wao. Hata hivyo, Messi amekiri kuwa ratiba ngumu ya mashindano imeanza kuonekana kwa wachezaji wake kutokana na kucheza mechi zenye ushindani mkubwa katika hatua za mtoano.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
“Huu ni mchezo wa kipekee kwangu. Ni mara yangu ya kwanza kucheza dhidi ya England. Ni taifa lenye historia kubwa katika soka la dunia, hivyo ni heshima kubwa kushiriki mechi ya kiwango hiki katika hatua ya nusu fainali,” amesema Messi baada ya ushindi huo.
Messi pia amesifu ari ya kikosi cha Argentina, akieleza kuwa licha ya kutwaa taji la Dunia na Copa América katika miaka ya karibuni, bado wachezaji wana njaa ya mafanikio zaidi. “Kikosi hiki hakikomi kupambana. Kila mara kinataka kufikia mafanikio makubwa zaidi. Tulichokifanya hadi sasa si jambo dogo, lakini bado tunaendelea kupigania zaidi,” amesema nahodha huyo.
Akizungumzia hali ya timu, nyota huyo ameweka wazi kuwa wachezaji wamechoka kutokana na ratiba nzito, lakini wanaendelea kujiandaa kwa mchezo dhidi ya England. Pia alimpongeza Julián Álvarez kwa bao lake zuri pamoja na Lautaro Martínez, akisisitiza kuwa Argentina inapaswa kuendelea na kiwango hicho ili kufikia fainali.


