Kocha wa Arsenal, Mikel Arteta, ameonyesha hasira kali kufuatia uamuzi wa kubatilisha penati iliyotolewa kwa timu yake katika sare ya 1-1 dhidi ya Atletico Madrid kwenye mkondo wa kwanza wa nusu fainali ya UEFA Champions League.
Tukio hilo lilitokea dakika za mwisho baada ya Eberechi Eze kuangushwa ndani ya boksi na beki David Hancko, ambapo mwamuzi Danny Makkelie alitoa penati kabla ya kubadilisha uamuzi wake baada ya VAR kuingilia kati.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Arteta alisema kwa hasira “Ninachokasirishwa nacho ni jinsi gani penati ya Eze imefutwa kwa namna ilivyofanyika. Hii inabadilisha kabisa mwelekeo wa mchezo katika kiwango hiki.”
Aliongeza kuwa “Tumewekeza nguvu nyingi kwa miezi tisa kufika hapa, haiwezekani kitu kama hiki kitokee katika hatua hii muhimu.”
Arsenal walitangulia kwa bao kupitia penati ya Viktor Gyökeres baada ya Hancko kumchezea rafu, kabla ya Julian Alvarez kusawazisha kupitia penati nyingine mapema kipindi cha pili baada ya VAR kuthibitisha mpira wa mkono wa Ben White.
Kwa upande wake, kocha wa Atletico Diego Simeone alisema anaunga mkono matumizi ya VAR, akisema: “VAR wakati mwingine inatoa na wakati mwingine inachukua, lakini lazima tukubali maamuzi yake.”
Matokeo hayo yanaacha kila kitu wazi kabla ya mchezo wa marudiano utakaochezwa London, huku timu zote mbili zikisaka kufuzu fainali ya kwanza ya Champions League katika historia yao. Simeone alihitimisha akisema “Tunakwenda London na matumaini makubwa, tutapigana kwa kila kitu tulichonacho.”


