Morgan Gibbs-White alitumia mitandao ya kijamii kutoa shukrani zake kwa mashabiki baada ya kupokea salamu nyingi za kumtakia heri kufuatia jeraha lake la kutisha kichwani dhidi ya Chelsea.

Kiungo huyo wa Nottingham Forest alichapisha picha akiwa na nyuzi kwenye paji la uso wake, huku ukubwa wa jeraha ukionekana wazi.
Jeraha hilo linamfanya awe na shaka kushiriki katika mechi ya marudiano ya nusu fainali ya UEFA Europa League dhidi ya Aston Villa siku ya Alhamisi. Akiandika kwenye Instagram, Gibbs-White alisema: “Asanteni kwa ujumbe wa kuonyesha upendo, ushindi mzuri sana, hongera Taiwo Awoniyi.”
Nottingham Forest waliondoka wakiwa mbele kwa pointi sita zaidi ya eneo la kushuka daraja la EPL baada ya ushindi mzuri wa 3-1 dhidi ya Chelsea uwanjani Stamford Bridge. Sasa wako kwenye msururu wa mechi 10 bila kupoteza katika mashindano yote.
Mshambuliaji Taiwo Awoniyi alifunga mabao pande zote za penalti ya Igor Jesus kuhakikisha pointi tatu zinapatikana. Forest walimpoteza mchezaji muhimu Morgan Gibbs-White kutokana na jeraha la kichwa kipindi cha pili, dakika 20 tu baada ya kuingia kama mchezaji wa akiba.

Kocha wa Nottingham Forest Nuno Espírito Santo alisema: “Nangoja. Morgan Gibbs-White ana jeraha la wazi (kidonda kikubwa kichwani) lakini ni mpambanaji na ana mtazamo imara. Natumai kitengo chetu cha matibabu kinaweza kufanya ‘miujiza’ ili kumweka katika hali ya kucheza dhidi ya Aston Villa. Tutaona.
“Nilimwambia: ‘Huhitaji kupiga kichwa mpira ili ucheze’. Anazungumza kawaida, anakumbuka kila kitu. Kitu pekee ni maumivu tutaona.”
Forest tayari walimkosa beki Zach Abbott baada ya kubadilishwa kwa sababu ya mtikisiko wa ubongo (concussion), kabla ya Morgan Gibbs-White kuondoka pia. Abbott naye aligongana kichwa. Kocha alisema: “Nilizungumza na Zach vyumbani. Nafikiri yuko sawa.”
Kocha huyo alikuwa amefanya mabadiliko manane kwenye kikosi chake cha kwanza dhidi ya Chelsea. Wachezaji kadhaa muhimu akiwemo Gibbs-White walikaa benchi, huku kocha huyo akitazama mchezo wa marudiano wa Alhamisi wakiwa na faida ya 1-0.
“Ninawafahamu vizuri sana wachezaji wangu. Nafanya nao kazi kila siku. Nilifanya hivyo pia tulipocheza dhidi ya FC Midtjylland na walicheza vizuri sana,” alisema.
“Kwa upande wangu nilijaribu kusawazisha nguvu ya timu. Tuna majeruhi. Niliamua kuwapa dakika 45 baadhi yao, kwa sababu dakika 45 tunaweza kupona ndani ya siku tatu ili kuwa fiti kwa mchezo dhidi ya Aston Villa.”



