Madrid, Hispania Rais wa Real Madrid, Florentino Pérez, amesababisha mjadala mkubwa ndani ya soka la Hispania baada ya kutangaza kupitia video ya kampeni kwamba José Mourinho atakuwa kocha mkuu wa klabu hiyo iwapo atashinda uchaguzi wa urais utakaofanyika Juni 7, 2026.
Pérez, ambaye anawania kurejea madarakani, alitoa kauli hiyo akisema kuwa “klabu inahitaji uongozi wenye nidhamu na ushindani wa kiwango cha juu.” Tangazo hilo limeelezwa na wachambuzi kama hatua ya kisiasa yenye lengo la kuongeza nguvu katika kampeni yake ya uchaguzi.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Hispania, Mourinho tayari amesaini mkataba wa miaka mitatu utakaomuweka Santiago Bernabéu hadi Juni 2029, ingawa utekelezaji wake unategemea ushindi wa Pérez katika uchaguzi huo unaotarajiwa kuwa mkali.
Mpinzani wa Pérez, Enrique Riquelme, amepinga vikali mpango huo akisema “Real Madrid inahitaji mradi wa muda mrefu, si maamuzi ya kihisia au ya haraka yanayotegemea majina makubwa.”
Uamuzi huo umekuja baada ya Real Madrid kumaliza msimu bila taji lolote na kukumbwa na mvutano ndani ya vyumba vya kubadilishia nguo. Pérez anaamini Mourinho ndiye mtu sahihi kurejesha nidhamu na makali ya ushindani katika kikosi chenye mastaa kama Kylian Mbappé, Vinícius Júnior, na Jude Bellingham.


