Mshambuliaji wa Simba SC, Elie Mpanzu, amefunguka hadharani kuhusu sababu iliyomshawishi kuongeza mkataba wa kuendelea kuitumikia klabu hiyo, akitaja upendo mkubwa kutoka kwa mashabiki kuwa ndio chachu kuu ya uamuzi wake.
Mpanzu alieleza kuwa katika kipindi kigumu alichopitia, mashabiki wa Simba walimpa sapoti ya kipekee iliyompa nguvu ya kuendelea kupambana na kurejea kwenye kiwango chake.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kupitia ujumbe wake, mshambuliaji huyo alisema “Nikiwa na machozi machoni mwangu ninawaandikia, wapenzi mashabiki wa Simba. Ninyi ndio wafuasi bora zaidi ambao nimewahi kukutana nao.”
Aliendelea kwa kusema “Nataka kuwashukuru kutoka moyoni mwangu kwa msaada wenu usioyumba, licha ya nyakati ngumu ambazo nimepitia. Mmekuwa mkiniamini kila wakati.”
Kwa kumalizia, Mpanzu alisisitiza uamuzi wake wa kubaki klabuni hapo akisema “Ndiyo maana nimeamua kutowasaliti na kuendelea na klabu. Ninawapenda nyote sana na ninawaahidi mambo mema katika siku zijazo.

