Mmiliki wa Nottingham Forest, Evangelos Marinakis anafikiria kumfukuza kocha Steve Cooper kama sehemu ya marekebisho makubwa katika Ligi ya Uingereza.
Katika kile kinachoweza kuwa mtikisiko mkubwa katika klabu hiyo, Mtendaji Mkuu wa Forest Dane Murphy pamoja na wafanyikazi wake wa kuajiri pia wako hatarini huku klabu ikifikiria kufanya marekebisho ya usimamizi.
Wakati wa Cooper anaonekana kukaribia kikomo huku Nottingham wakiwa mkiani mwa Ligi kufuatia kichapo cha 4-0 Jumatatu usiku kutoka kwa Leicester City, ikiwa ni kupoteza kwao kwa mechi tano mfululizo katika ligi kuu msimu huu.
Hata hivyo, kwa mujibu wa Sportsmail inafahamu kwamba baada ya paundi milioni 150 kutumika kununua wachezaji 22 wakati wa majira ya joto, vigogo wengine katika klabu hiyo wanaweza pia kuondoka wiki hii.
Mtendaji mkuu wa Nottingham Marekani Murphy, mkuu wa kitengo cha uajiri George Syrianos na skauti Andy Scott wote wako kwenye mstari unaowezekana wa kufutwa kazi huku wamiliki wa klabu hiyo wakitathmini hali ilivyo na kutafuta kuboresha udhaifu wao.
Murphy, 36, kiungo wa zamani wa New York Cosmos, alijiunga na Nottingham kutoka Barnsley lakini maoni yake yamechunguzwa zaidi katika wiki za hivi karibuni na anatarajiwa kufanya mazungumzo na Marinakis huku kukiwa na wasiwasi kwamba wanahitaji uzoefu zaidi.
Mtendaji mkuu wa zamani wa Newcastle United Lee Charnley amekuwa akisaidia Nottingham kwa ushauri na bado anaweza kuhojiwa kama mbadala wake iwapo hatua madhubuti itachukuliwa.
Mmiliki huyo alikuwa na mkutano wakatriwa chakula cha jioni na Cooper huko London Jumamosi jioni huku akisisitiza haja ya uboreshaji wa haraka.
Cooper alikuwa mkweli katika kutathmini kikosi chake kufuatia kushindwa kwa Forest dhidi ya Leicester na anasalia kuwa maarufu miongoni mwa wafuasi. Anatambua kwa urahisi hitaji la mabadiliko katika viwango vya utendakazi na anatumai atapewa muda zaidi.
Rafa Benitez alitajwa kuwa anaweza kuchukua nafasi ya Cooper iwapo ataondoka lakini Mhispania huyo, ambaye alifanya kazi mara ya mwisho kwenye Premier League akiwa na Everton, anafikiriwa kutovutiwa na kazi hiyo katika Uwanja wa City Ground. Vyanzo vya habari vilisema Jumanne kwamba Mhispania huyo hajafuatwa rasmi na klabu ya Midlands.
Cooper alipewa mkataba mpya na Forest katika majira ya joto baada ya kuiongoza klabu hiyo kurejea ligi daraja la kwanza msimu uliopita.