Klabu ya Newcastle United imefikia makubaliano na Hoffenheim ya Ujerumani kumsajili winga mahiri wa Ivory Coast, Bazoumana Toure, katika dirisha hili la usajili.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 aling’ara katika msimu wa 2025/26 wa Bundesliga, akichangia kwa kiwango kikubwa Hoffenheim kumaliza nafasi ya tano na kufuzu kucheza michuano ya Europa League. Katika mechi 30 za ligi, Toure alifunga mabao matano na kutoa pasi tisa za mabao.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kwa mujibu wa mwandishi wa habari za usajili, David Ornstein wa The Athletic, Newcastle imefanikiwa kufikia makubaliano na Hoffenheim, huku mchezaji huyo akitarajiwa kusafiri kuelekea Tyneside kwa ajili ya vipimo vya afya kabla ya kukamilisha uhamisho wake.
Newcastle ilianza kutafuta winga mpya wa kushoto baada ya Anthony Gordon kujiunga na Barcelona kwa ada ya takribani Euro milioni 70. Awali, klabu hiyo ilitarajia kumsajili Victor Munoz kutoka Osasuna, lakini Liverpool iliingilia kati na kukamilisha usajili huo kwa kulipa kipengele chake cha kuachiliwa cha Euro milioni 40.
Inaelezwa kuwa Newcastle sasa iko tayari kuwekeza Euro milioni 50 ili kuhakikisha inamnasa Bazoumana Toure, ambaye ameonekana kuwa mmoja wa wachezaji waliovutia zaidi katika Bundesliga msimu uliopita. “Newcastle imefikia makubaliano na Hoffenheim kwa ajili ya usajili wa Bazoumana Toure, na mchezaji huyo anatarajiwa kusafiri kwa ajili ya vipimo vya afya kabla ya kukamilisha uhamisho wake,” ameripoti David Ornstein wa The Athletic.


