Gerard Pique anatumaini Barcelona watamshawishi Lionel Messi kuendelea kubaki katika klabu hiyo ya Spain kwa miaka mingi ijayo.
Messi, mwenye umri wa miaka 33 alionesha hisia zake kwa kuomba kuihama hiyo miamba ya LaLiga wakati wa kumaliza msimu uliyopita, lakini jaribio lake liligonga mwamba na kuendelea kusalia katika klabu hiyo.
Lakini, mshindi huyo wa tuzo ya Ballon d’Or mara sita amekuwa akihusishwa vilabu kama Manchester City, Paris Saint-Germain na Inter mara baada ya kumaliza kwa mkataba wake.
Lakini Pique anatumaini Messi atasalia Barcelona ambako ametumia maisha yake yote ya soka la kulipwa.
“Tutatakiwa kumuomba Messi. Ni maamuzi yake binafsi… na tutaona nini kitatokea,” beki huyo aliiambia Radio Marca siku ya Ijumaa.
“Nina amini kwa kuwa anaendelea kuvaa jezi ya Barca basi kuna tumaini.
“Tunaamini watamshawishi kwa hiyo atakaa kwa miaka mingi.
Messi amekuwa akipambana sana msimu kuwa katika fomu yake ya kawaida msimu huu, amefunga magoli sita peke katika mechi 11 magoli matatu ni kutoka kwenye michezo nane Laliga.
Messi hajafanikiwa kutengeneza asisti katika LaLiga wakati pia ana wastani 2.1 wa kutengeneza nafasi kwa dakika 90, rekodi duni tangu mwaka 2012-13.
Hadi 130,000,000 TSH Kutolewa kwa washiriki wa shindano la Playson Cashfall. Unaipata kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet Pekee. Jisajili sasa, kisha ingia mchezoni kabla ya Novemba 29.




Shakila mrope
Ata mm pia napenda abakie barca
Dorophina
Messi akibakia barca itakuwa poa sana
Rahma
Nic
Adelta
Messi ni mzalendo wa Barcelona tu
Nasra
Messi na Barcelona damdam
Hopemwaikuka
Hata mm na wish hvyo
Sabrina
Messi Barcelona For life
Magdalena
Messi amalizie kucheza soka tu Barcelona
Sauda
Messi bora abaki Barcelona
Issa
Mess ni wa barca tu
Ester jackson
Wachezaji mwezake messi wanamuhitaji ingawa viongozi mda mwingine wanajifanya hawamuhitaji kumbe wanatamani aendelee back
Fatina mfingi
Nice
Janeflora malisa
Safi
Tatu
Mess bora abaki Barcelona
samiah
Safi
warda
Ila wangemuacha abadili upepo