Kocha wa Marekani, Mauricio Pochettino, ameipongeza timu yake kwa umoja na uimara baada ya kushinda Bosnia na Herzegovina kwa mabao 2-0 wakiwa na mchezaji 10 tu uwanjani, lakini akapinga vikali uamuzi wa kadi nyekundu aliyopewa mshambuliaji Folarin Balogun.
Balogun, ambaye alifunga bao lake la tatu kwenye mashindano hayo, alitolewa nje baada ya tukio la kugusa kifundo cha mguu cha mchezaji wa Bosnia Tarik Muharemović, lakini Pochettino alisema tukio hilo lilikuwa la bahati mbaya na halikustahili adhabu hiyo kali.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
“Hii haikuwa kadi nyekundu kamwe. Nilipoitazama kwenye TV, hakuna nia yoyote ya kumkanyaga mchezaji,” alisema Pochettino.
Kocha huyo alisisitiza kuwa tukio hilo lilitokea kwa bahati mbaya na ni sehemu ya kawaida ya mpira wa miguu, akiongeza kuwa Balogun alikuwa na huzuni lakini bado anajivunia kufuzu kwa hatua inayofuata ya mashindano. “Ilikuwa ni tukio la kawaida tu la mpira. Ilitokea kwa bahati mbaya, si kwa makusudi, na ndiyo maana kwangu haikuwa kadi nyekundu,” aliongeza.
Ushindi huo umeiwezesha Marekani kufuzu kwa hatua ya 16 Bora, ambapo wataumana na Ubelgiji, huku Pochettino akipata mafanikio ya kuwa kocha wa kwanza wa timu ya taifa ya Marekani kushinda mechi tatu katika mashindano ya Dunia.


