Prince Dube Namba Hazidanganyi

Prince Dube amekua mtambo wa mabao ndani ya kikosi cha Yanga SC ambacho kimefunga raundi ya 30 kwa ubao kusoma Yanga SC 5-0 Dodoma Jiji, Juni 22 huku akiwa na hatihati kuukosa mchezo wa Kariakoo Dabi, Juni 25 2025, Uwanja wa Mkapa.

Prince Dube Namba Hazidanganyi

Prince Dube ambaye hakuwa sehemu ya mchezo dhidi ya Dodoma Jiji baada ya kupata maumivu kwenye mchezo wa raundi ya 28 dhidi ya Tanzania Prisons uliochezwa Juni 18 2025, Uwanja wa Sokoine, Mbeya.

Kwenye mchezo huo Dube alikomba dakika 22 nafasi yake ilichukuliwa na Clatous Chama ambaye alifunga bao moja dakika ya 35 akitumia pasi ya Clement Mzize wakati ubao ukisoma Tanzania Prisons 0-5 Yanga SC.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Ndani ya ligi namba nne kwa ubora, Prince Dube kafunga mabao 13 akitengeneza pasi 8 za mabao ikiwa ni msimu wake wa kwanza kuwa ndani ya kikosi cha Yanga SC.

Prince Dube Namba Hazidanganyi

Prince Dube ni mchezaji wa kwanza kufunga hat trick msimu wa 2024/25 alifunga kwenye mchezo dhidi ya Mashujaa uliochezwa Uwanja wa KMC Complex.

Yanga SC imefunga jumla ya mabao 81 baada ya mechi 29 ikiwa ni timu namba moja kufunga mabao mengi. Dube kahusika kwenye mabao 21.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.