Rabiot: Hatuogopi Hispania, wala hatuna mpango maalum wa kumzuia Yamal

Kiungo wa Ufaransa, Adrien Rabiot, amesema kikosi cha Les Bleus hakiogopi Hispania wala hakijapanga mbinu maalum za kumzuia nyota wa Barcelona, Lamine Yamal, kuelekea nusu fainali ya michuano ya Dunia. Rabiot amesema maandalizi ya timu yake yamejikita katika kuikabili Hispania kama timu nzima badala ya kumlenga mchezaji mmoja.

Rabiot: Hatuogopi Hispania, wala hatuna mpango maalum wa kumzuia YamalAkizungumza kabla ya mchezo huo mkubwa, Rabiot alisema: “Hakuna mpango wa ‘anti-Yamal’. Tunaiangalia Hispania kwa ujumla wake, si mchezaji mmoja. Ni timu yenye hatari kila sehemu ya uwanja, hivyo tunapaswa kudhibiti mfumo wao wa uchezaji badala ya kumlenga mtu mmoja.”

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Rabiot pia alieleza kuwa kikosi cha Ufaransa kinaingia kwenye mechi hiyo kikiwa na imani kubwa baada ya safari nzuri iliyokuwa nayo kwenye mashindano. “Hatuogopi mtu yeyote. Kwa namna tulivyofika hapa, naamini tuko katika hali bora kabisa. Uwanja ndio utaamua matokeo, lakini sisi tumefanya kila linalowezekana kuwa tayari, alisema.

Rabiot: Hatuogopi Hispania, wala hatuna mpango maalum wa kumzuia YamalKiungo huyo alibainisha kuwa siri ya mafanikio ya Ufaransa ni umoja uliopo ndani ya kikosi. “Tuna uhusiano mzuri sana nje ya uwanja na hilo limetupa nguvu kubwa. Pia tunajua hii ndiyo mashindano ya mwisho kwa kocha wetu akiwa na timu ya taifa, jambo ambalo linatupa motisha ya ziada kupigania ubingwa,” aliongeza.

Rabiot: Hatuogopi Hispania, wala hatuna mpango maalum wa kumzuia YamalRabiot alisisitiza kuwa mawasiliano ya karibu kati ya wachezaji yamekuwa nguzo muhimu ya mafanikio yao. Tunazungumza sana sisi kwa sisi, tunachambua mechi pamoja na kushirikiana mawazo. Wote tuna lengo moja na tunapambana kuelekea upande mmoja, jambo ambalo linaonekana wazi katika michezo yetu,” alisema.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.