Rangnick Aanza Vyema na Timu ya Austria

Kocha mpya wa timu ya taifa ya Austria Ralf Rangnick ameanza kwa ushindi mnono na timu ya taifa ya Austria kwa kuicharaza 3-0 Croatia katika michuano ya UEFA Nations League ya mwaka huu.

Baada ya kumaliza muda wake na klabu ya Manchester United Rangnick ilisemekana ataendelea kushirikiana na United akiwa kama mshauri wa klabu lakini baadaye alipiga chini majukumu hayo na kuangazia zaidi majukumu ya ukufunzi na timu ya taifa ya Austria.

Rangnick amekuwa kocha wa kwanza wa Austria kuiongoza kupata ushindi na clean sheet tangu mwaka 2002 ambapo Hans Krankl alikuwa kocha timu hiyo.

Akizungumza baada ya mchezo kumalizika, Rangnick alisema alifurahishwa na jinsi timu yake ilivyokabiliana na Croatia na kuibuka ushindi.

“Tulikuwa na matatizo katika dakika 25 za kwanza, lakini kupata bao la kuongoza kabla ya mapumziko kulitusaidia vyema,” alisema.

“Kipindi cha pili tulicheza vizuri sana na tukafunga mabao mawili mazuri – tungeweza kufunga zaidi.

“Nimeridhika sana.”


SHINDA SAMSUNG A32 NA AVIATOR

SHINDA Samsung A32 ukiwa na mchezo wa Aviator kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet! Kwea pipa ukusanye zawadi zako pamoja na ushindi mnono wa mkwanja!

kasa wa njano, Kasa wa Njano Awapa Ubingwa wa CL Liverpool., Meridianbet

SOMA ZAIDI HAPA

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.