Real Madrid Yaandaa Ofa Nono Kwa Michael Olise

Real Madrid inatajwa kujiandaa kuwasilisha ofa ya pauni milioni 130 kwa Bayern Munich katika jitihada za kumsajili winga wa kimataifa wa Ufaransa, Michael Olise. Mabingwa hao wa Hispania wanaonekana kumuweka nyota huyo juu ya orodha yao ya usajili baada ya msimu wake bora akiwa Bundesliga.

Real Madrid Yaandaa Ofa Nono Kwa Michael OliseKwa mujibu wa taarifa mbalimbali za soka Ulaya, Rais wa Real Madrid, Florentino Pérez, anataka kumleta Olise kama moja ya zawadi zake za kwanza kwa kocha José Mourinho. “Perez anaamini Olise anaweza kuwa sehemu muhimu ya mradi mpya wa Real Madrid na kuongeza ubora katika safu ya ushambuliaji,” zimeeleza taarifa hizo.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Hata hivyo, Bayern Munich imeweka wazi msimamo wake kuhusu mchezaji huyo. Rais wa heshima wa klabu hiyo, Uli Hoeness, amesisitiza kuwa nyota huyo hayupo sokoni na kwamba viongozi wa Bayern hawana mpango wa kujadili uhamisho wake. “Olise ni sehemu ya mipango ya muda mrefu ya Bayern Munich na hatuko tayari kumpoteza,” inaelezwa kuwa ndiyo msimamo wa mabingwa hao wa Ujerumani.

Real Madrid Yaandaa Ofa Nono Kwa Michael OliseMbali na kukataa mawazo ya kumuacha aondoke, Bayern pia inaripotiwa kuandaa mpango wa kumuongezea mshahara ili kuimarisha uhusiano wake na klabu hiyo. Olise bado ana mkataba wa kuitumikia Bayern hadi mwaka 2029, hali inayowapa nguvu viongozi wa klabu hiyo katika mazungumzo yoyote yatakayojitokeza.

Real Madrid Yaandaa Ofa Nono Kwa Michael Olise
Nyota huyo wa Ufaransa amekuwa na msimu wa kuvutia uliomfanya kutunukiwa tuzo ya Mchezaji Bora wa Kifaransa anayecheza nje ya Ufaransa. “Ubunifu wake, uwezo wa kupiga chenga na mchango wake wa mabao umemfanya kuwa mmoja wa mawinga wanaohofiwa zaidi barani Ulaya,” zimeeleza ripoti hizo, huku vita vya usajili kati ya Real Madrid na Bayern vikitarajiwa kuwa moja ya gumzo kubwa la dirisha hili la usajili.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.