Winga wa England, Bukayo Saka, amesema timu yao ina kila sababu ya kuamini inaweza kutwaa taji la Dunia 2026 kutokana na ubora wa kikosi, ari ya ushindani na uzoefu walioupata katika michuano mikubwa ya hivi karibuni.
Akizungumza katika kambi ya England jijini Kansas City kabla ya mchezo wao wa kwanza dhidi ya Croatia, Saka alisema kushiriki fainali mbili za Euro na kufika robo fainali ya Kombe la Dunia 2022 kumewajengea wachezaji imani kubwa ya kufanya vizuri zaidi safari hii. “Nadhani somo kubwa tulilojifunza ni kuwa na imani. Ukiangalia kikosi chetu unaona kipaji, ari na kujiamini tulivyonavyo,” alisema Saka.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Mchezaji huyo wa Arsenal alieleza kuwa England pia ina viongozi bora na wachezaji wenye uzoefu wa kushinda mataji, jambo ambalo linaweza kuwa silaha muhimu katika safari yao ya kutafuta ubingwa wa dunia. “Tuna washindi wa kweli na viongozi wa kweli ndani ya timu. Kwa imani hiyo, naamini tunaweza kupiga hatua inayofuata,” aliongeza.
Saka alisema hali ya kambi ya England kwa sasa ni nzuri na kila mchezaji ana hamasa kubwa ya kuanza mashindano hayo. “Nimefurahi sana. Wachezaji wote wako katika hali nzuri na mazingira ya kambini ni mazuri. Tunasubiri kwa hamu mchezo wetu wa kwanza na kuanza rasmi mashindano,” alisema.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 pia alibainisha kuwa ubingwa wa Ligi Kuu England alioutwaa akiwa na Arsenal msimu uliopita umempa kujiamini zaidi. “Mimi na wachezaji wengine kutoka Arsenal tunaingia Kombe la Dunia tukiwa na uhuru na kujiamini zaidi, na naamini hilo litatusaidia kuboresha kiwango chetu,” alihitimisha.


