Nahodha wa Misri, Mohamed Salah, amesema aliamua katika sekunde za mwisho kupiga penalti ya mtindo wa Panenka wakati wa mikwaju ya penalti dhidi ya Australia, hatua iliyosaidia taifa lake kutinga hatua ya 16 bora ya mashindano ya Dunia kwa ushindi wa penalti 4-2 baada ya mchezo kumalizika kwa sare ya 1-1 ndani ya dakika 120 nchini Marekani.
Salah, ambaye alicheza mchezo mzima licha ya kusumbuliwa na majeraha madogo ya msuli wa nyuma ya paja, alisema alihisi ni wajibu wake kubeba jukumu hilo kutokana na uzoefu wake mkubwa ili kuwapa wenzake kujiamini katika wakati mgumu wa mchezo. “Kama kuna mtu alipaswa kufanya hivyo, basi nilipaswa kuwa mimi. Nina uzoefu zaidi kuliko wengine na nilitaka kuwapa wenzangu kujiamini. Niliamua katika dakika ya mwisho, ilibidi nifanye hivyo,” alisema Salah.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Nyota huyo wa zamani wa Liverpool amesema ushindi huo umeandika historia kwa Misri, ambayo imefanikiwa kushinda mchezo wa hatua ya mtoano ya michuano ya Dunia kwa mara ya kwanza. Amesema amewahimiza wachezaji wenzake kufurahia mafanikio hayo kwa kuwa ni tukio la kipekee katika historia ya soka la taifa hilo.
“Kila mara ninajaribu kufurahia kila wakati kwa sababu haujirudii. Nimewaambia wenzangu wafurahie wakati huu. Hatujawahi kuvuka hatua ya makundi wala kufuzu hatua inayofuata, hivyo huu ni wakati wa kusherehekea,” alisema.
Kocha wa Misri, Hossam Hassan, ambaye kabla ya mchezo alikuwa na mashaka kuhusu utayari wa Salah kutokana na jeraha, alimjumuisha katika kikosi cha kwanza. Misri sasa itakutana na Argentina ya Lionel Messi katika hatua ya 16 bora, huku Salah akiwa tayari amechangia bao moja na pasi mbili za mabao katika mashindano hayo.


