“Sasa ni Muda Wetu”– Saka Afunguka Baada ya Arsenal Kutwaa Ubingwa wa EPL

Mshambuliaji wa Arsenal na timu ya taifa ya England, Bukayo Saka amesema kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu England kumewanyamazisha waliokuwa wakiibeza klabu hiyo kwa miaka mingi, baada ya Arsenal kumaliza ukame wa miaka 22 bila taji hilo.

“Sasa ni Muda Wetu”– Saka Afunguka Baada ya Arsenal Kutwaa Ubingwa wa EPL
Saka alisema aliwahi kupitia kipindi kigumu mwaka 2020 wakati Arsenal ilikuwa nafasi ya 15 kwenye msimamo wa ligi, hali iliyomfanya aandike ujumbe wa huzuni kwa mashabiki kwenye mtandao wa X akisema walistahili zaidi kutokana na kiwango kibovu cha timu hiyo kipindi hicho.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

“Tulikuwa kwenye kipindi kigumu sana, watu walikuwa wanatutania na kutucheka kila mahali, lakini sasa yote yamekwisha. Hakuna mchezo tena, sasa ni muda wetu,” alisema Saka.

“Sasa ni Muda Wetu”– Saka Afunguka Baada ya Arsenal Kutwaa Ubingwa wa EPLNyota huyo alisema kutwaa ubingwa huo baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Crystal Palace katika Uwanja wa Selhurst Park ilikuwa kama ndoto iliyotimia kwa wachezaji wa Arsenal.

“Sasa ni Muda Wetu”– Saka Afunguka Baada ya Arsenal Kutwaa Ubingwa wa EPLKiungo Declan Rice naye alisema maneno ya kuwapa moyo wachezaji baada ya kupoteza dhidi ya Manchester City yalisaidia kuibadilisha Arsenal, huku kikosi cha Mikel Arteta kikishinda mechi zote zilizobaki na kutwaa ubingwa huo kwa tofauti ya pointi saba dhidi ya City ya Pep Guardiola.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.