Nahodha wa Ubelgiji, Youri Tielemans, amesema anajivunia mchango wake baada ya kuiongoza timu yake kutoka nyuma kwa mabao mawili na kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Senegal, matokeo yaliyoipeleka Ubelgiji hatua ya 16 Bora ya michuano ya Dunia.
Tielemans, ambaye ni kiungo wa Aston Villa, alifunga mabao mawili muhimu katika mchezo huo. Romelu Lukaku aliifungia Ubelgiji bao la kwanza la kurejea mchezoni kabla ya Tielemans kusawazisha, kisha akafunga bao la ushindi kwa mkwaju wa penalti baada ya kuangushwa na Lamine Camara kufuatia ukaguzi wa VAR.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
“Kuwa sehemu ya comeback hii ni jambo la kujivunia kwa sababu nilifunga mabao mawili ya mwisho. Najivunia sana na kufanikisha timu kuvuka hatua hii,” alisema Tielemans baada ya mchezo.
Katika kipindi cha pili, kulizuka mvutano kati ya Tielemans na mwenzake Leandro Trossard, lakini baada ya mapumziko mafupi ya kunywa maji, wawili hao walirejea kushirikiana vyema na kuchangia kurejesha matumaini ya Ubelgiji.
“Tunafurahi kubaki hapa Seattle kwa sababu kutokuwa na safari nyingi kunaweza kutupa faida kubwa katika mechi zinazofuata,” alisema Tielemans, huku Ubelgiji ikisubiri kumfahamu mpinzani wake kati ya Marekani au Bosnia & Herzegovina katika hatua ya robo fainali.


