Kocha wa Chelsea, Thomas Tuchel ameeleza kuwa anaamini sana kuwa atafanikiwa kushinda taji la UEFA msimu huu atakapocheza na Manchester City baadae mwezi huu.
Chelsea na Manchester City watakutana tena katika fainali ya Champions league tarehe 29 mwezi huu. Bado haijajulikana ni uwanja gani utatumika kutokana na ule wa awali kule Instabul kutiliwa shaka baada ya Uturuki kuwekewa vikwazo na Uingereza.
Katika mahojiano maalum, Tuchel alisema kuwa ushindi waliopata dhidi ya Manchester City juzi umewatengenezea hari na imani kubwa ya kuchukua ubingwa wa UEFA toka wafanye hivyo mwaka 2012 dhidi ya Bayern Munich.
“Ndiyo, mchezo huu umetupa imani kubwa ya kushinda fainali dhidi ya City, na tunaamini tunaweza kufanya hivyo kama tulivyofanya nyuma. Tutajaribu kutunza hali tuliyonayo ya kujiamini tutakapofika Istanbul, kwani tutakuwa na lengo moja tu la kushinda taji hilo” alisema Tuchel
Tuchel pia aliongeza kuwa michezo wanayocheza hivi sasa itawaanda zaidi kuelekea kwenye fainali hiyo kubwa ambayo mashabiki wa the Blues walikosa kwa muda mrefu.
Hii ndiyo burudani yenye ushindi! Ingia kwenye kasino ya Meridianbet kufukuzia ushindi huu. Cheza sasa Lucky Lucky na uwe moja ya washindi na Mabingwa.
Chelsea msijiamini sana jamani
Kila la kheri Chelsea
Chelsea mko makini San nawaaminia
Safi sana
Vizuri
Safi sana
Chelsea msijiamini Sana mkumbuke huu ni mpira lolote linaweza tokea
Kazeni buti Chelsea
Safi sana
Wapambane watachukua.
Safii sana
Hsitakua mechi lahisi
Imani ndo Jambo la msingi sana
Kila la kheri