Waziri wa Elimu ya Awali na Michezo wa Morocco, Mohamed Saad Berrada, ameibua mjadala mkubwa miongoni mwa mashabiki wa soka barani Afrika baada ya kusisitiza kuwa timu ya taifa ya nchi hiyo inacheza kwa ajili ya Morocco pekee na si kwa niaba ya bara la Afrika katika michuano ya Dunia.
Akizungumza kuhusu ushindani wa kimataifa, Berrada alisema kila taifa lina wajibu wa kutetea maslahi yake na heshima ya wananchi wake bila kubeba jukumu la kuwakilisha bara zima. “Tunacheza kwa ajili ya Morocco si kwa ajili ya Afrika, kila taifa lina jukumu la kupigania heshima yake,” alisema waziri huyo.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kauli hiyo imekuja wakati Morocco ikiwa miongoni mwa mataifa ya Afrika yanayoshiriki mashindano ya Dunia, hali ambayo kwa miaka mingi imekuwa ikifanya mashabiki kutoka nchi mbalimbali za Afrika kuziunga mkono timu za bara hilo zinapofika hatua za juu za mashindano.
Baadhi ya wachambuzi wa soka wameeleza kuwa kauli hiyo inaonyesha mtazamo wa utaifa katika michezo ya kimataifa, ambapo kila nchi huweka mbele mafanikio yake. Hata hivyo, wengine wanaamini kuwa mafanikio ya taifa moja la Afrika katika jukwaa la dunia huongeza pia heshima ya bara zima.
Mjadala kuhusu kauli ya Berrada umeendelea kushika kasi kwenye mitandao ya kijamii, huku baadhi ya mashabiki wakitafsiri maneno hayo kama ishara ya kupungua kwa mshikamano wa bara la Afrika. Wengine, hata hivyo, wameitetea Morocco wakisema kuwa katika mashindano ya kimataifa kila taifa lina haki ya kuweka mbele maslahi na utambulisho wake wa kitaifa.


