Bosi wa timu ya taifa ya Uingereza Gareth Southgate atatoa nafasi kwa wachezaji makinda waweze kuonesha walicho nacho pale Wales itakapo tembelea viunga vya Wembley jioni ya leo (Saa nne kamili usiku saa za afrika mashariki).
The Three Lions, watajipima ubavu na majirani zao Wales kuulekea katika michuano ya Nations League kwa ratiba itakayo ikutanisha Uingereza na Belgium na Denmark.
Straika wa Everton Dominic Calvert-Lewin anajiandaa kucheza mchezo wake wa kwanza katika timu ya wakubwa baada ya kuwa na moto katika msimu mpya wakati mchezaji mwenzake ambaye pia ni mgeni Buyako Saka na Harvey Barnes naye pia anatarajiwa kuchezeshwa.
Jack Grealish na Conor Coady wote ndani ya kikosi hii ni baada ya kufanya vizuri katika mchezo wa kwanza walipocheza dhidi ya Danes mwezi uliyopita, magolikipa Nick Pope na Dean Henderson watakuwa kando kumsaidia golikipa namba moja Jordan Pickford.

Timu ya Ryan Giggs,Wales ambao ni wageni wa Uingereza hajapoteza katika michezo nane iliyopita watafanya mabadiliko kutokana kukosekana kwa idadi kubwa ya wachezaji.
Gareth Bale bado hajawa fit kucheza, wakati Joe Allen,Hal Robson-Kanu na Tom Lockyer wote wanauguza majeraha.
The Dragon itamkosa pia kiungo wao Aaron Ramsey, ambaye anatumikia muda wa kujitenga akiwa Juventus baada ya watumishi wawili wa klabu hiyo ya Turin kukutwa na maambukizi ya COVID-19.
Southgate atalazimika kuwakumbusha tena vijana wake majukumu yao wakati wakiwa wanawakilisha taifa lao la Uingereza.
Tammy Abraham,Ben Chilwell na Jadon Sancho wataukosa mchezo huu baada ya kuvunja sheria za Kujikinga na COVID-19 kwa kufika sehemu zenye mikusanyiko ya watu wengi zaidi ya sita wiki iliyopita lakini pia Greenwood na Phil Foden wameachwa katika kikosi cha Southgate.

Ingawa matokeo ya leo hayana umuhimu sana lakini Southgate anatarajia matokeo chanya kutoka katika timu yake baada ya kuwa na kiwango kibovu mechi dhidi ya Iceland na Denmark.
Je Wajua?
England haijapoteza katika michezo nane ya kirafiki tangu ilifungwa 3-2 na Ufaransa mwaka 2017.The Three Lions imeruhusu magoli mawili pekee katika michezo yote nane.
Raheem Sterling amefunga magoli 11 katika mechi 13 za England lakini ameshindwa kuvamia nyavu katika michezo 17 ya kirafiki.
Wales wameshinda mara moja pekee katika mechi 17 walizokutana na England katika dimba la Wembley ushindi wao huo mmoja waliupata mwaka 1977 goli pekee lililofungwa na Leighton James kwa mkwaju wa penati.
Sasa unaweza kuweka pesa moja kwa moja kwenye akunti yako ya Meridianbet kwa kutumia mtandao wa Airtel. Usipate wasi wasi, tunaifanya kazi kuwa rahisi zaidi!



magdalena
itakuwa bonge la mechi
Caroline
Asante kwa taarifa
Fatina mfingi
Itakuwa game
lombo
game kali sana
Adelta
Hii Ni bonge la mechi
Lydia Emmanuel Magoti
Bonge la game hilo
Angelina
Game kali
Amiri Kayera
Plan yake nzur san
Fatuma kasomo
Bonge la game
Juliana Alex
Mtanange matata sana
Rehema
Bonge la makala
Sadick
England ya Southgate imekuwa na kikosi kipana na wachezaji mahiri wanaotakiwa kufanya kiti kwa mashabiki wenye wazimu wa mpira wa England wenye hamu kuona taifa lao linarudia historia ya mwaka 1966 ilipochukua Ubingwa wa dunia#meridianbettz
Theonestina
Itakuwa mechi ya kibabe
Sabrina
Itakua hatarii
aisha
Shuhuli itakua nzito maana wales hatokubali kizembe apigwe hapo ndio itakua kazi ipo
Gabriel
Mtanange mkal sana 👍
felister
kazi itakuwepo
Rose kapinga
Wote wababe
Dorophina
Mtanange utakuwa sio wa kitoto mechi zote kali
Mwajumah
Itakua bonge la mechi
Samiah
Duuuh hptoshi
Sauda
Mechi ngumu
Tatu
His machi itakuwa kali
Janeflora malisa
🔥
Nasra
Bonge la game
Ernest
England huenda wakafanya makubwa safari hii
Shani
England win
Venerose
Wales win
Saupha mohamed
Mechi kalii
Samira
England msimu huu wapo motooo
Issa
England ni shida ingine tena
Povel
Don’t miss
Hopemwaikuka
Hii si ya kuikosa kabsa
David Pere
England ya Southgate imekuwa na kikosi kipana na wachezaji mahiri wanaotakiwa kufanya kiti kwa mashabiki wenye wazimu wa mpira wa England wenye hamu kuona taifa lao linarudia historia ya mwaka 1966 ilipochukua Ubingwa wa dunia