Van Dijk Apigwa Faini na FA

Nahodha wa Liverpool Virgil Van Dijk ameongezewa adhabu ya mchezo mmoja na faini ya paundi laki moja baada ya kukiri  kutoa maneno makali kwa mwamuzi baada ya kuoneshwa kadi nyekundu kwenye mchezo wa ligi kuu ya Uingereza dhidi ya Newcastle.

Beki Van Dijk alitolewa kwa kadi nyekundu katika mchezo dhidi ya Newcastle baada ya kufanya madhambi, Lakini wakati anatoka alionekana akitoa maneno kwa mwamuzi jambo ambalo limemfanya kufungiwa na kupigwa faini.VAN DIJKAdhabu ya beki huyo wa kimataifa wa Uholanzi ilikua imalizike katika mchezo ambao aliukosa na klabu yake ya Liverpool kushinda kwa mabao matatu dhidi ya Aston Villa hivo beki huyo ataukosa mchezo dhidi ya Wolves utakaopigwa Septemba 16.

Mchezaji huyo baada ya mahujiano alikiri kua alitoa maneno ya matusi kwa msimamzi wa mcheza na shirikisho la soka nchini Uingereza kuamua kumpa adhabu beki huyo wa kimataifa wa Uholanzi baada ya kukiuka kanuni za ligi hiyo.VAN DIJKKukosekana kwa beki Van Dijk katika mchezo mwingine inaendelea kua pigo kwa klabu ya Liverpool, Kwani  beki huyo amekua muhimili mkubwa klabuni hapo tangu atue kwenye timu hiyo mwezi Januari mwaka 2018 akitokea Southampton.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.