Nahodha wa West Ham United, Jarrod Bowen, anaweza kulazimika kufanya uamuzi mkubwa kuhusu mustakabali wake wa soka msimu huu wa kiangazi ikiwa timu hiyo itashuka daraja kutoka Ligi Kuu England.
West Ham wanaingia kwenye mchezo wao wa mwisho wa msimu dhidi ya Leeds United wakiwa kwenye vita ya kusalia EPL, huku vilabu kadhaa vikubwa vikionesha nia ya kumhitaji Bowen. Inaelezwa kuwa Bowen bado ana nia ya kuendelea kubaki West Ham iwapo timu hiyo itaepuka kushuka daraja Jumapili hii. Hata hivyo, kushuka kwenda Championship kunaweza kubadilisha kabisa hali hiyo.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya klabu, wachezaji wa West Ham wana kipengele cha kupunguziwa mshahara kwa asilimia 50 iwapo timu itashuka daraja, jambo ambalo linaweza kuifanya klabu ishindwe kuzuia ofa kubwa kwa nyota wake huyo.
Bowen, ambaye alikosa nafasi kwenye kikosi cha Thomas Tuchel cha England kuelekea Kombe la Dunia, ameendelea kuvutia vilabu vingi kutokana na uwezo wake wa uongozi na mchango mkubwa wa mabao na mashambulizi.
“West Ham hawatamuuza Bowen kwa bei rahisi hata kama watashuka daraja. Thamani yake bado ipo juu kutokana na kiwango chake bora cha muda mrefu katika Premier League.”
Mshambuliaji huyo mwenye miaka 29 ana mkataba hadi mwaka 2030, lakini anatarajiwa kuvutia ofa nyingi kutoka vilabu vya EPL iwapo West Ham watashindwa kubaki ligi kuu. Inaelezwa kuwa Bowen angependa kubaki jijini London iwapo ataondoka West Ham, huku Tottenham Hotspur ambao wanaweza kubaki EPL kwa gharama ya West Ham mwishoni mwa wiki hii wakitajwa kuwa miongoni mwa vilabu vinavyofuatilia hali yake. Vilabu vingine vinavyomuwania ni Chelsea, Liverpool na Newcastle United.
West Ham watalazimika kuifunga Leeds United katika Uwanja wa London Stadium na wakati huo huo kutegemea Everton kuifunga Tottenham ili kuhakikisha wanabaki kwenye Ligi Kuu England msimu ujao.


