Baada ya kusubiri kwa muda wa siku 1,727 bila kuwa kwenye majukumu ya ukocha, gwiji wa soka Zinedine Zidane anaripotiwa kufikia makubaliano ya awali na shirikisho la soka French kuchukua nafasi ya ukocha mkuu wa timu ya taifa ya timu ya taifa ya France.
Taarifa zinaeleza kuwa Zidane anatarajiwa kuanza rasmi kazi hiyo baada ya kumalizika kwa michuano ya kombe la Dunia 2026, akimrithi Didier Deschamps ambaye ameiongoza timu hiyo tangu mwaka 2012.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Katika kipindi chake, Deschamps ameandika historia kwa kuiongoza Ufaransa kutwaa ubingwa wa kombe la Dunia 2018, pamoja na kuiweka timu hiyo katika ushindani mkubwa kimataifa.
Rais wa FFF, Philippe Diallo, amethibitisha kuwa tayari wana jina la kocha ajaye, huku Deschamps mwenyewe akisisitiza kuwa muda wake umefika mwisho ifikapo mwaka 2026.
Iwapo uteuzi huo utakamilika, Zidane atakabidhiwa jukumu zito la kuendeleza mafanikio ya “Les Bleus”, huku mashabiki wengi wakisubiri kuona kama ataweza kurudisha enzi ya mafanikio aliyowahi kuwa nayo akiwa mchezaji na kocha.

