Matumaini ya Cristiano Ronaldo kuibuka mfungaji bora mbele ya Ciro Immobile katika soka ya Bara Ulaya msimu huu yanazidi kupotea, baada ya kushindwa kutikisa nyavu za wapinzani katika mchuano ulioshuhudia waajiri wake Juventus wakichapwa 2-0 na Cagliari.
Nyota huyo matata mzawa wa Ureno anajivunia mabao 31 kutokana na kampeni za Ligi Kuu ya Italia (Serie A) hadi kufikia sasa msimu huu.
Licha ya Juventus kuonekana kutamalaki mechi na kuwazidi maarifa wapinzani wao katika takriba kila idara, ni Cagliari ndio waliotumia vyema uwanja wao wa nyumbani na kuvuna ushindi muhimu.
Mabao ya kikosi hicho yalifumwa wavuni na Luca Gagliano na Giovanni Simeone katika dakika ya 8 na 45 mtawalia.
Ronaldo kwa sasa anahitaji mabao manne zaidi ili kumfikia Ciro Immobile wa Lazio katika vita vya kuwania taji la mfungaji bora miongoni mwa wanasoka wote wa ligi za bara Ulaya msimu huu.
Immobile alifunga bao lake la 35 msimu huu mnamo Jumatano ya Julai 29 katika mechi iliyowashuhudia Lazio wakiwapepeta Brescia 2-0.
Ikisalia mechi moja pekee kabla ya kampeni za Serie A kutamatika rasmi msimu huu, Immobile ndiye anapigiwa upatu kuibuka mfungaji bora wa bara Ulaya.
Bao lake la hivi karibuni lilimwezesha kumpiku Robert Lewandowski wa Bayern Munich aliyefunga rasmi kampeni za Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga) kwa magoli 34.
Immobile kwa sasa anasalia na bao moja pekee kufikia rekodi ya Gonzalo Higuain aliyewahi kufunga idadi kubwa zaidi ya mabao katika msimu mmoja wa Serie A.
Higuain alipachika wavuni mabao 36 akivalia jezi za Napoli mnamo 2015-16.
Nini kinachokupa raha kama michezo ya kasino ya mtandaoni? Hasa unapojua kuwa kuna ushindi, jackpot na mizunguko kibao ya bure.
Ungana na bwana Meridian kupata ushindi na burudani.
Mwajumah
Ciro apambane tu atafika anapopataka#Meridianbettz
Sadick
Bado serie A zimabaki mechi mbili kila timu kumaliza msimu, lolote linaweza kutokea. Pamoja na mafanikio ya Ciro Immobile,Lewandowsk, Ronaldo na Benzema bahati mbaya msimu huu Ballon D’Or imefutwa#meridianbettz
Dorophina
Naamini cr7 lazima ataibuka kidedea kufikisha magoli mengi
Adelta
Ciro aongeze juhudi
#meridianbettz
Antony Luseno
Bora Ciro awe ndo apewe tuzo isiwe mazoea kila msimu majina ni yale yale yaliyozoeleka
Mwanahamisi
Ciro aongeze juhudi
Magdalena
Aongeze juhudi aendelee kukaza Buti atafika malengo
Lydia Emmanuel Magoti
Navyo mjua Ronaldo akubaligi kushindwa kabisa atafanya afanyavyo mpaka afike pale panapo stairi
Khadija
Aendelee kukaza buti atafika malengo#meridianbettz
Zeiyana
Ciro immobile ni mchezaji hanayekuja na kasi ya hajabu sana kila kitu kinawezekana kikubwa hawe na nia tu asikate tamaa
Caroline
Ciro Immobile anakuja vizuri
Sauda
Ciro akaze buti
Fatina mfingi
Aongeze juhudi na apende anachokifany!!
Janeflora malisa
Aongezee bidiii
Fatuma kasomo
Aongeze juhudi tu
Ernest
Ciro amaekuwa kwenye kiwango kizuri sana msimu huu hivyo anastahili kutwaa kiatu cha dhahabu cha Italia
Shafii
Immobile yuko vizuri Sana na anapokua dimbani hua anajituma Sana lengo lake kuakikisha nyavu za timu pinzani zinatikisika.
Tatu
Akuna na washindana na cr7
Isaya massawe
Kwa namna hii Rinaldo lazima apigwe bao na ciro
Samira
Ciro ameonyesha kiwango kizuri sasa hvi
Sylvester
Ciro Immobile ndio atakua kinara wa magoli kwani Ronaldo kwa hii mechi moja iliyobakia hawezi kufikia magoli ya Ciro Immobile
marry
apamabne zaid
Rehema
Habari mzuri
Furahav
Habari nzuri
Issa
Immo ni mchezaji mahiri eneo la 18 hivyo imemfanya afunge mabao mengi season hii
Devotha
Ciro aongeze juhudi aipeke kazi yake na aiheshimu pia atafanya vizuri zaidi
Hope mwaikuka
Pambana tu
Gabriel
Habar njema
Tahiya
Daah nilikuwa na matumaini na Ronaldo kupata kiatu ila ndio Ciro naye amepambana
lombo
duh ajitahid tu
farida ahmadi
Kwa hiyo Cristian Ronaldo ndio amekosa hiyo tuzo da siamin
Saupha mohamed
Good news
Sabrina
Akaze buti tu atapata
Salma ngende
Good
Genia Sikaluzwe
Akaze buti atafkia malengo
Latifa juma mohamed
Aongezee juhud
David Pere
Sababu bado mechi moja Kama atakaza kesho atachuku kiatu Cha ufungaji Bora ulayaa
Theckla
Japo mechi zimebaki chache ila lolote linaweza tokea
Omary lukumbi
Ciro immobile amekua na msimu bora sana ndan ya kikosi cha lazio
tumaini
Maoni:Habari njema
Povel
Hapo wote wakal game ya mwixho ndo itahamuan nan mshindi
Rose kapinga
Safiii
felister
ajitahidi atafikia malengo lakini sidhani kama Christian Ronald anaweza mwachia iv iv
Amiri Kayera
Wanashindan kwer
Asia Abdy
Wakomae
Ester jackson
Cr7 msimu huu hana bahati
warda
Hongera yake Ciro mana kapata