Licha ya kuiongoza Juventus kutwaa ubingwa wa Serie A msimu uliopita, Maurizio Sarri alijikuta akitimuliwa Juventus baada ya kutolewa kwenye Ligi ya Mabingwa na Lyon.
Mengi yalisemwa kutokana na tukio hilo na sasa aliyewahi kuwa mchezaji wa Juventus, Mirallem Pjanic amefunguka na kudai Sarri hakuwaamini wachezaji wake wa Juventus.
Raisi wa Juventus – Andrea Agnelli alinukuliwa akisema kulikuwa na kutoelewana kati ya Sarri na wachezaji nyota wa timu hiyo na hivyo ilibidi mmoja aondoke.
Akizungumza na Tutto Sport, Pjanic ambaye alikuwa miongoni mwa wachezaji wa Juventus chini ya kocha huyo, alinukuliwa akisema ” Sarri hakuwa anawaamini wachezaji wake, na hilo lilinisumbua sana.
“Kila mchezaji kwenye timu ile alikuwa anajitoa kwa ajili ya timu. Unaweza usielewane na mtu mmoja au wawili lakini muda mwingine watu wanakosea.
“Japokuwa, hili halijawahi kuharibu kiwango chetu. Wachezaji wato ni wazuri na wanahitaji ushindi. Lakini, kama kocha ataanza kuharibu hili ndio kinatokea alichokizungumza raisi.
“Hakuna mtu aliyewahi kuwa na mashaka na uwezo wake kama kocha, lakini kulikuwa na hili tatizo. Mwisho wa siku, tulileta kombe nyumbani, kitu ambacho huwezi kukichukulia poa.”
Juve walibeba kombe kwa tofauti ya pointi 1 dhidi ya Inter Millan japokuwa mashabiki wa timu hiyo hawakupendezwa na namna ya uchezaji wa timu hiyo.
Ondoka na Mkwanja Kwenye Tsh. 160,000,000
Hii ndiyo burudani yenye ushindi! Ingia kwenye kasino ya Meridianbet kufukuzia ushindi huu.
Issa
Sarr kocha mzuri sema hana bahat
Aziza mushi
Ni kocha mzuri tu.
Povel
Sarri hanaga jipya kwny soka vilabu vyote alivyopita vyote katimulawah tu
Hopemwaikuka
Imeeleweka
Janeflora malisa
Ttz hana nyota
aisha
Hana maajabu huyo
Theonestina
Duuuh
Elika
Ishakuwa shida kwake sasa
Khadija
Kwa nn? sasa anakosa kuwaamin
Adelta
Asante kwa taarifa meridian
zeiyana
Sarr ni kocha mzuri ila hakua na maelewano mazuri na wachezaji wake
Mwanahamisi
Duuh
Lydia Emmanuel Magoti
Namkubali Sana huyo kocha anajua nini anakifanya
Tatu
Kocha mwenye maamuzi yake ayumbichwi
Sauda
Sarri hana jipya
Saupha mohamed
Duuuh
Fatuma kasomo
Kocha yupo vizuri
Sabrina
Sarri ni kocha makini sana
Asia Abdy
Nice
Neema
Kocha yuko vzr sana
warda
Ila hawakufanya poa kwa kweli
Latifa juma mohamed
Daaah!!
David Pere
Namkubali Sana huyo kocha anajua nini anakifanya
Ernest
Sarr ni kocha mzuri sema kwa msimu wa mwaka jana Juve walimuangusha kocha wao