Huyu Chama Weka Mbali na Watoto  

KIUNGO wa Simba Clatous Chama kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Dodoma Jiji, pasi zake asilimia 88 alitumia kutoa kwa mguu wa kulia.

Jumla nyota huyo alitoa pasi 87, alitumia mguu wa kushoto kutoa pasi 7 na ule wa kulia alitumia kutoa pasi 87.

Mguu wake wa kulia una shida kubwa katika matumizi akiwa uwanjani kwa kuwa unawapa tabu wapinzani wake na una nguvu kwa upande wake.

Kwa upande wa uwezo wa kukukota alifanya hivyo mara 19 na alipiga kona 5 ikiwa ni dakika ya 40,46,47,66 na 81. Alitoa pasi moja ya bao ambalo lilifungwa na Ninja wa Dodoma Jiji ambaye alijifunga kwa pigo la kichwa.

Simba ilishinda mabao 3-0 Dodoma Jiji na watupiaji wengine walikuwa ni Moses Phiri ambaye anafikisha mabao manne pamoja na Habib Kyombo ambaye anafikisha mabao mawili ndani ya ligi.

Acha ujumbe