Beki wa zamani wa Chelsea FC, César Azpilicueta, ametangaza rasmi kuwa atastaafu soka la ushindani mwishoni mwa msimu huu baada ya kucheza kwa zaidi ya miaka 20 katika kiwango cha juu.
Azpilicueta, ambaye kwa sasa anaitumikia Sevilla FC, alithibitisha taarifa hiyo kupitia ujumbe wa hisia alioutoa Ijumaa asubuhi, akieleza kuwa ulikuwa wakati mgumu kwake kuandika barua ya kuaga mchezo huo alioupenda maisha yake yote.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
“Leo nataka kushiriki nanyi kwamba msimu huu utakuwa wa mwisho kwangu kama mchezaji wa kulipwa. Baada ya miaka mingi ya kuishi ndoto yangu, nahisi umefika wakati wa kuanza ukurasa mpya wa maisha yangu,” alisema Azpilicueta.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 36 alisema hakuwahi kufikiria kuwa angekuwa na safari kubwa kiasi hicho tangu alipokuwa mtoto akicheza mpira mjini Pamplona nchini Spain. Pia aliwashukuru watu wote waliokuwa sehemu ya mafanikio yake ndani na nje ya uwanja.
Katika kipindi chake cha miaka 11 ndani ya Chelsea, Azpilicueta alicheza zaidi ya mechi 500 na kushinda mataji makubwa tisa, jambo lililomfanya kubaki kuwa mmoja wa wachezaji wenye heshima kubwa katika historia ya klabu hiyo ya London Magharibi.


