WAKIWA na kazi ya kusaka ushindi kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al Ahly, Waarabu wa Misri uongozi wa Simba SC umebainisha kuwa kambi yao ya Zanzibar itakuwa tiba nzuri dhidi ya Wapinzani wao hao, kwa mujibu wa Mkuu wa Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo Ahmed Ally.
Timu hiyo inaiwakilisha Tanzania kwenye anga la kimataifa katika Ligi ya Mabingwa Afrika, mchezo wao wa hatua ya robo fainali unatarajiwa kuchezwa Machi 29 Uwanja wa Mkapa. Odds kubwa, kasino ya mtandaoni na michezo ya sloti ni njia rahisi ya kukupa mtonyo mrefu. Ingia mchezoni hapa.
Mshindi kwenye mchezo wa kwanza atakuwa ametanguliza mguu mmoja hatua ya nusu fainali ambayo itaamuliwa kwenye mchezo wa nusu fainali ya kwanza itakayochezwa Misri.
Ahmed Ally, Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba SC ameweka wazi kuwa kambi hiyo ni maalumu ambayo waliianza Jana Machi 19, 2024 ni kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrka dhidi ya Al Ahly. Beti na Meridianbet kwa odds kubwa na machaguo kibao, pia unaweza kubashiri mubashara.
“Tutakuwa na mchezo dhidi ya Al Ahly ambao ni wa Ligi ya Mabingwa Afrika tunahitaji kuwa na utulivu mkubwa kuelekea mchezo huo na malengo ni kuona kwamba tunapata matokeo mazuri.
“Kambi ya Zanzibar hii itampa muda mwalimu kuwafundisha wachezaji kwa utulivu na kuwa tayari kuelekea mchezo wetu dhidi ya Al Ahly, inawezekana kupata matokeo na muda ni sasa kwa ajili ya maandalizi hayo,”.
Kikosi cha Simba kimeondoka Machi 19 kuelekea Zanzibar kwa ajili ya kambi ya muda inayotarajiwa kuwa ni muda wa siku 7 mpaka 8. Jisajili na Meridianbet upate bonasi za kasino kibao na odds kubwa za ubashiri kwa machaguo kibao.