UONGOZI wa Azam FC umebainisha kuwa kwenye anga la kimataifa wanaimani watafanya kitu kikubwa ambacho kitawashangaza wengi ambao hawana imani na timu hiyo.
Ipo wazi kwamba Azam FC itapeperusha bendera ya Tanzania kwenye anga la kimataifa baada ya kugotea nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 69.Hasheem Ibwe, Ofisa Habari wa Azam FC ameweka wazi kuwa kila kitu kipo kwenye mpango bora na walikuwa wanahitaji kushiriki Ligi ya Mabingwa Afrika.
“Tulianza msimu kwa mpango kazi kutokana na kile ambacho kilikuwa kwetu na wengi hawakutarajia kwamba tutakuwa hapa na imetokea kwa kuwa tunakwenda kimataifa tutafanya kitu.“Mpango wa mwanzo ilikuwa kufanya vizuri kwenye ligi ya ndani imekuwa hivyo na sasa tunakwenda kwenye anga la kimataifa tutafanya vizuri kwa kuwa mipango ipo vizuri.”
This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.
Strictly Necessary Cookies
Strictly Necessary Cookie should be enabled at all times so that we can save your preferences for cookie settings.
If you disable this cookie, we will not be able to save your preferences. This means that every time you visit this website you will need to enable or disable cookies again.